Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Yussuf Haji Khamis

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Nungwi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. YUSSUF HAJI KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, nachukua fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema ya uhai na uzima. Pia nakushukuru wewe kwa nafasi hii ya kuchangia katika Wizara hii ingawa kwa ufupi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze mchango wangu kwa kupongeza chombo hiki muhimu kwa ulinzi uliotukuka wa mipaka ya nchi yetu na kutoa nafasi kwa wananchi kushiriki kazi za ujenzi wa Taifa kwa amani na utulivu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumze Kambi ya Jeshi Mtoni-Zanzibar. Kambi ya Jeshi Mtoni ipo ndani ya Mji wa Unguja. Kambi hii kwa mtazamo wangu mazingira yake siyo mazuri kiusalama kwani uzio uliozunguka kambi hivi sasa umeanza kuvamiwa baadhi ya sehemu zake. Upande wa Kusini wa uzio tayari umevamiwa na watu kwa shughuli za kibinadamu kama maduka, baa, car wash na kadhalika. Huduma hizi zinafanywa na watu mbalimbali usiku na mchana. Naomba Waziri anieleze shughuli zile ni za Jeshi au za nani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wanajeshi wetu waliovamiwa Congo na kupoteza askari 14 na wengi kujeruhiwa vibaya kwa kiasi wameathirika kisaikolojia, nataka kujua lini watarejeshwa nchini ili warudi katika hali zao?