Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, karakana za jeshi; nipende kushauri Serikali kuhakikisha kufufua karakana za nyumbu ambazo wakati wa Mwalimu Nyerere Nyumbu ilishaanza kuunda mpaka magari yake ukiacha matengenezo ya kawaida na uchongaji wa vyuma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Nyumbu Kibaha ilisaidia kuajiri vijana wetu wengi ambapo kwa sasa hali ya karakana haiko sawasawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuongeza ajira kwa vijana wetu kupitia JKT. Nashauri Serikali kuangalia kwa upya juu ya wale vijana 2000 ambao walichukuliwa operation Kikwete kwa ahadi ya kuajiriwa. Mbaya zaidi walipomaliza na kuingia utawala mwingine wale wote waliokuwa nyuma, utawala huu haukujali kuwaajiri, walianzisha operation nyingine ambayo imemaliza mkataba wake wa kujenga Mererani na kuahidiwa kuajiriwa mara moja kwa kauli ya Rais. Je, wale walioko mitaani na ujuzi wa silaha hatuji kuleta hatari pale ambapo watashindwa maisha na kuamua kuingia katika uhalifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha za fidia, nashauri Serikali kulipa fidia kwa wananchi ili kuweza kukidhi mahitaji yao ili kupunguza minong’ono iliyojaa uraiani inayopunguza mshikamano na wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zabuni na ulipaji wa zabuni. Nashauri Serikali kuhakikisha wazabuni waliohudumia majeshi yetu kulipwa kwa wakati ili kutowapelekea wazabuni hao kuuziwa dhamana zao na mabenki kwa kushindwa kulipa mikopo yao.