Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, chonde chonde Jeshi letu lisiingizwe kwenye siasa za nchi hii, kazi yao kulinda mipaka na raia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ku-define upya mipaka ya majeshi kwani maeneo mengi yamevamiwa na raia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jeshi litumike kujenga uchumi, mashamba maalum, kikosi maalum cha utafiti wa masuala kadha wa kadha ambayo ni changamoto kwa nchi yetu. Jeshi liboreshewe makazi yao wengine wanakaa kwenye majumba yaliyochakaa. Uundaji wa magari ya Nyumbu uliokuwa umekua kwa kiasi kikubwa uliishia wapi? Wanajeshi ndio nguzo ya nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maduka ya jeshi bei rahisi ni ya muhimu sana kupunguza gharama za maisha na kuwafanya wanajeshi kuishi kwa shida.