Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchukua fursa hii kumpongeza kwa dhati Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, kwa kazi nzuri ya kuliongoza Taifa katika kulinda amani na utulivu ikiwemo kulinda mipaka yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpongeza Waziri na Wataalam wote wa Wizara katika kudumisha amani na usalama kwa kushirikiana na nchi nyingi duniani. Napenda kusisitiza umuhimu wa mafunzo ya jeshi kujikita katika mafunzo ya maadili na uzalendo. Mafunzo haya ni muhimu sana katika ustawi wa nchi yetu pia jeshi letu kuendelea kuwa na heshima hapa kwetu na nje ya Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua mchango na umuhimu wa askari wetu katika masuala ya ulinzi na usalama na hasa katika mchango wa ukombozi wa Bara la Afrika. Nashauri askari wastaafu waongezewe maslahi yao kulingana na hali ya sasa. Pia kuna Askari waliopata ulemavu wakiwa katika majukumu yao, napendekeza wapewe maslahi mazuri kutokana na kujitoa kwao kulinda nchi yetu na pia ukombozi wa Afrika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napendekeza makambi yetu muhimu ikiwemo Kambi ya Mbalizi, kuyaweka katika mkakati wa kuyatafutia maeneo nje ya Miji. Kambi za Jeshi kwa nje ya Miji na makazi ya watu ni muhimu sana kiusalama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napendekeza Serikali kuboresha huduma za hospitali za Jeshi kwa vile ni muhimu sana kwa huduma za askari na pia raia, hospitali za Jeshi letu zina sifa nzuri ya huduma kwa wananchi na kwa kuboresha zitapata ngazi nzuri na heshima za kimataifa. Napendekeza kuwepo mafunzo endelevu katika Jeshi letu ikiwemo mafunzo ya teknolojia za kisasa na kiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.