Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ulinzi wa amani, Askari wetu hasa Wanajeshi wanaotumwa kwenda nchi za nje kusaidia kulinda, wamekuwa wakipoteza maisha yao huko nje, wanarudi maiti na familia zao zinapata shida. Naiomba Serikali iwafikirie wajane na familia za wanajeshi hao wanaofariki kwenye mapambano ili wapate pensheni hadi wanapofariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ajira. Kuna vijana wapatao 2,000 waliahidiwa kupata ajira kwenye Jeshi lakini hadi sasa vijana hao hawajaajiriwa. Naiomba Serikali iwapatie kipaumbele vijana wetu walioahidiwa kupata ajira wapate ajira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ulinzi mipakani; kumekuwa na tatizo la ulinzi mipakani watu wamekuwa wakiuawa lakini Serikali inasema kuna usalama. Naiomba Serikali ichukue hatua za haraka kudhibiti vifo hivyo. Wanajeshi wetu wapewe vifaa vya kutosha ili wafanye kazi nzuri huko mipakani kulinda mipaka ili kupunguza vifo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wanajeshi kutumika kwenye siasa. Wanajeshi wamekuwa wakitumika kwenye siasa. Mfano, Wanajeshi kutumika kwenye kupokea Madiwani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, matukio ya ugaidi. Kuna matukio mengi yanayoashiria ugaidi, watu wamekuwa wakiuawa, wakipotea wakati Majeshi yetu yapo. Naiomba Serikali idhibiti mauaji hayo na upotevu huo kupitia Wanajeshi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu SUMAJKT; niwapongeze kwa kazi nzuri ya ujenzi wa shule ya sekondari huko Bukoba. Wametumia ubunifu kutumia fedha ndogo iliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari hiyo. Naomba Wanajeshi hao waongezewe bajeti ya maendeleo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.