Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniruhusu nami nichangie hii Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Kwanza leo nina furaha sana pale kwenye nafasi ya Wageni wa Mheshimiwa Spika, wako watu muhimu sana. Walikuwepo watu muhimu sana, Jenerali Sarakikya, alikuwepo Jenerali Mbona, Jenerali Waitara, Jenerali Mwamunyange na Mheshimiwa Jenerali Mabeyo. Katika nchi nyingine huwezi kupata mfumo wa namna hii wa kukaribishana majeshini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kila kiongozi wa jeshi aliyeondoka, ameondoka na mgogoro mkubwa sana. Ni Tanzania tu ndipo unaweza kuona mfumo huu na hii inaashiria nini? Maana yake ni amani na usalama. Jambo hili ni geni katika nchi nyingine, limejengwa, halikuja tu Tanzania, maana yake kuna viongozi wamefanya kazi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Mheshimiwa Zungu amenifilisi, lakini yako machache ambayo ni muhimu nami niyachangie, mojawapo likiwa la pongezi kwa majeshi yetu. Majeshi yetu yanafanya kazi kubwa sana huko nje, yanasifiwa sana. Ila kama wanavyosema watu kwamba Masihi hasifiwi kwao, sisi hapa kwetu tunasahau Vita ya Kagera. Leo mtu anasimama hapa anaongelea negative ya Vita vya Kagera. Kaenda kutembelea makumbusho ya Vita ya Kagera. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ku-declare interest, mimi nilikuwa Operation Kagera na nina medali ya Vita vya Kagera, mimi na mke wangu. Ukienda pale siyo mahali pa kuangalia negative, ni mahali pa kusifia. Vita ile ni sifa kubwa ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania, siyo la kubeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, liko tatizo ambalo limejitokeza hapa la kuwekewa ceiling jeshi katika matumizi yake. Jeshi lisiwekewe ceiling na wanasiasa au Waziri wa Fedha aweke ceiling ya matumizi ya Jeshi. Ni vigumu sana kutambua matumizi ya Jeshi. Jeshi linabadilika na hali ya dunia, teknolojia, electronic warfare ndiyo inayochukua nafasi. Tanzania hatukuwa na miundombinu ya electronic warfare, maana ndiyo kwanza inakuja. Lazima Serikali ijiandae kutoa hela nyingi kujenga miundombinu ya electronic warfare. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi ulinzi katika dunia yote unahusu mambo ya defence, siyo kupigana physically. Hakuna mtu anayetaka kwenda vitani, ila kila mtu anataka kuzuia vita. Huwezi kuzuia vita kwa maneno ya bajeti ya shilingi mbili tatu. Jeshi linahitaji hela na Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Serikali nzima tujue kwamba tunataka Jeshi imara lenye weledi na usasa, haliwezi kuwa hivyo bila kupewa hela. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali hii itoe hela kuyasema yote, kuyatekeleza yote ambayo Mheshimiwa Zungu ameyataja, yanahitaji hela. Mkono mtupu haulambwi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ipo issue mbaya sana. Sera ya Sheria ya Ulinzi wa Taifa, imekaa miaka chungu nzima Zanzibar, wenzetu waipitie tu kwa nini hairudi hapa, kwa nini haiji Bungeni ikajadiliwa hiyo sera? Naomba Kiti hicho kitumike, kwamba Bunge liiombe Serikali ilete sera hiyo hapa tuijadili ili kuboresha Sheria ya Ulinzi wa Taifa, ni muhimu sana na tukichelewa ni adhabu mbaya tutawapa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wangependa sera hii ijadiliwe upungufu wote ambao umetajwa kwamba Majenerali wanaostaafu, mishahara tofauti imo ndani ya Sera ya Ulinzi wa Taifa ambayo imekwama Zanzibar. Zanzibar kuna nini, huo Muungano una nini, hawataki ulinzi Zanzibar? Hebu Bunge liisimamie Serikali kuleta hiyo sera humu ndani haraka iwezekanavyo.
kutoka SUMA JKT wakidhani wamepewa bure, imetimia bilioni 40 ni hela nyingi sana. Wakilipwa kidogo hata nusu wao pia matrekta hayo wameyakopa huko yalikotoka hawakupewa bure. Naomba Serikali isimamie suala hili, kuna Halmashauri zimetajwa pale, Geita na wapi warudishe hizo hela walizokopa kwenye matrekta, najua wameyauza lakini hela hawakurudisha, walete hela za SUMA JKT. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, liko suala dogo la SUMA Guards. SUMA Guards ni walinzi, lakini hapa nchini kuna sekta ya ulinzi binafsi inafanya kazi hizo zinazofanywa na SUMA Guards. Tatizo la SUMA Guards ambalo limejitokeza ni kwamba watu wanaopewa huduma ya SUMA Guards wanafikiri Serikali inatoa bure kama vile inavyofanya walivyokuwa wanalinda Mgambo au Jeshi la Polisi, hawawalipi SUMA Guards. Matokeo yake madeni yamekuwa makubwa na SUMA inachelewa kupanuka. SUMA Guards kingekuwa chombo kizuri cha kutegemewa hapa nchini, lakini wanabanwa kwa sababu hawalipwi wanafanya kazi bure. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati tumesema sana, wamejitahidi kukusanya hela kidogo, lakini wangeweza kupanuka zaidi kama wangekuwa wanalipwa madeni yao. Kwa hiyo, ushauri ni kwamba wapate zabuni, wasiitwe njooni mlinde hapa, wasiende, kwa sababu mtu anawaita hivyo hana bajeti, lakini anayetangaza zabuni ana bajeti ya zabuni hiyo kama ambavyo makampuni mengine ya ulinzi yanapata zabuni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kumekuwa na malalamiko ya chini chini na hili tuliseme wazi. Makampuni ya sekta ya ulinzi binafsi yanalalamika kwamba SUMA Guard wanapendelewa. Kwa vile wataomba zabuni watapata zabuni kwa ushindani, suala hili la kupendelewa litakufa, itakuwa jiwe moja ndege wawili. Kwanza watapata hela lakini kwamba wanapata kazi bure itafutika vilevile. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwamba Mheshimiwa Zungu alinifilisi....

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga hoja mkono. Ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee yako madeni ya SUMA JKT ya matrekta, watu wamekopa matrekta