Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na mchango wa maneno, naomba pia kuchangia kwa maandishi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2017 nilichangia na kuitaka Serikali ianze kutoa leseni kama sheria inavyotaka ili wananchi waweze kupata fursa ya kuweza kujiongezea kipato, kwa kuuza pombe ya Nipa ambayo ni by product ya mazao ya korosho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Nipa tumeweza kupata ethanol, methanol na alcohol ambayo inaweza kutumika viwandani. Haya yanafanyika sana nchi jirani ya Mozambique. Hivyo, Watanzania wanavusha hiyo Nipa na kupeleka nchi jirani ambayo wanatumia kujiingizia pesa za kigeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la Viwanda vya Korosho Masasi na maeneo mengine. Taarifa ya mwisho inasema kuna kesi Mahakamani, lakini katika hali ya kushangaza, viwanda hivyo sasa hivi vinatumika kama maghala na watu hao wanajipatia kipato wakati Serikali inasubiri kesi Mahakamani. Sasa ni wakati muafaka kesi hizi ziishe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mwisho kabisa ni kuhusu stakabadhi ghalani na commodity exchange. Kila mara taratibu hizi huwa zinaanza mikoa ya Kusini. Ni kwa nini? Kwa mfumo wetu wa sasa, commodity exchange kwa Tanzania kwenye mazao ya kilimo ni bado kabisa. Hivi karibuni watu wa TMX wamewaandikia barua wamiliki wa maghala ili waje kukutana nao. Kimsingi watu hawa wanataka kulazimisha wakati maandalizi hayajafanyika. Kwa hiyo,

tunaomba suala la commodity exchange likafanyike kwenye mazao mengine. Sasa naelewa kwa nini Mzee Nandonde (Mbunge wa zamani wa Tandahimba) aliomba Mtwara ijitenge. Kwa nini hakuna mikakati ya uhakika na kuwekeza viwanda?