Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa mchango wangu kwa Wizara hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni upi hasa mkakati wa Wizara kuhakikisha viwanda vyetu vya ndani vilivyojengwa, vinavyojengwa na vitakavyojengwa baadae vinalindwa ili viweze kukua na kuweza kuhimili ushindani wa viwanda vya wenzetu wa Ulaya, Asia na Amerika ambao viwanda vyao vimejiimarisha? Kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri hakuna mahali popote alipotaja kulinda viwanda dhidi ya ushindani usio haki kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wenye viwanda vya nguo, nyama, maziwa, nyanya na kadhalika wanalalamika juu ya ushindani usio haki unaotokana na waagizaji wa bidhaa toka nje kutolipa kodi stahiki kwa Serikali kwa sababu waagizaji hao wana-under declare ama kwa kushirikiana na watumishi wasio waaminifu wa TRA wanafanya under-valuation ya bidhaa walizoagiza na hivyo kulipa kodi isiyo stahiki. Nini nafasi ya Tume ya Ushindani katika hili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukumbuke kuwa sisi bado ni nchi changa sana, tusipokuwa na mkakati wa uhalisia wa kulinda viwanda vyetu, tusahau kabisa kuwa na uchumi wa viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naitaka Serikali ilete mpango mkakati wa kulinda viwanda vyetu ili ndoto ya Tanzania ya viwanda iweze kukamilika na kukuza uchumi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja ya Waziri, lakini lazima uzingatie kulinda viwanda vyetu.