Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 1992 Tanzania ilikuwa na viwanda 156. Viwanda hivi Serikali iliposhindwa kuviendesha ilivibinafsisha, lakini haviendelezwi. Kwenye hotuba ya Waziri hakuna mahali popote alipozungumzia chochote kuhusu waliobinafsishiwa viwanda na kutokuviendeleza. Tunaomba anapohitimisha hoja aje na majibu yanayoelekeza hatua zilizochukuliwa juu ya tukio hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, imesemwa Tanzania ni nchi ya viwanda, je, ni viwanda vya kuchuja alizeti na kutengeneza pipi? Mbona sioni juhudi ya Serikali juu ya viwanda vya kutengeneza nguo ukizingatia tunahimiza zao la pamba lilimwe kwa wingi? Nafikiri ni wakati muafaka wa viwanda vyote vya nguo mfano Urafiki, Mwatex, Mutex na kadhalika vifufuliwe kwa kuwa tunahimiza Watanzania kulima pamba ili malighafi yetu itumike na hapa kwetu kwa wingi pia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti yote inayopitishwa kwenye Bunge lako juu ya viwanda haionekani utekelezaji wake. Je, Tanzania ya viwanda itakuja kihewahewa? Tunaomba majibu kutoka kwa Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda Waheshimiwa Wabunge tunapoishauri Serikali hoja zote zichukuliwe, zifanyiwe kazi ili kuleta tija ya maendeleo katika Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna Mbunge yeyote asiyetaka maendeleo katika Taifa lake, ndiyo maana wote huchangia hoja kwa hisia. Hivyo hoja zifanyiwe kazi.