Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Yosepher Ferdinand Komba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. YOSEPHER F. KOMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanga viwanda vingi vimekufa kifo kitakatifu, Viwanda vya Chuma, Viwanda vya Mbolea, Viwanda vya Mafuta ya Kujipaka na kadhalika. Katika hotuba yako hakuna mkakati wowote wa kufufua viwanda mkoani Tanga. Naomba utakapohitimisha nipate maelezo kuhusu masuala yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kiwanda cha Matunda Tanga ambacho kilipangwa kujengwa Segera ili kiweze kukusanya matunda ya Muheza, Lushoto na Handeni, je, ni lini na wapi Kiwanda cha Matunda kitajengwa Tanga?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Muheza Kata Magorofo kuna shamba kubwa la michikichi ambalo linakufa kwa kukosa kiwanda cha kukamua. Je, ni lini Serikali itafufua kiwanda cha kukamua mawese kwa ajili ya upatikanaji wa ajira kwa wananchi na bidhaa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mkakati gani wa kushughulikia matatizo ya wafanyakazi, viwandani ambayo nayo kwa asilimia fulani yanachangia kufa, mfano wafanyakazi wa viwanda vya chai, Tarafa ya Amani.