Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kumshukuru Mungu kwa kunipa afya njema inayoniwezesha kutoa mchango katika sekta zinazosimamiwa na Wizara hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri wa Wizara hii Mheshimiwa Mwigulu Lameck Nchemba na Naibu wake pamoja na Makatibu Wakuu na wafanyakazi wote wa Wizara hii kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kuendeleza Sekta za Kilimo, Mifugo na Uvuvi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kujielekeza kwenye tathmini ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2015/2016 kwa sehemu ya bajeti ya maendeleo ambapo hadi tarehe 30, Aprili, 2016 kiasi cha shilingi 5,192,797,589/= tu zimetolewa kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo ikiwa ni asilimia 15.9 ya fedha zilizoidhinishwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, hali hii ya kutopeleka kwa wakati fedha za maendeleo zinaweza kufifisha jitihada ya kuleta mapinduzi ya kilimo itakayopelekea uzalishaji wa malighafi zitakazotumika kwenye viwanda, ambacho ndiyo kipaumbele cha Serikali hii ya Awamu ya Tano.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali nashauri ijitahidi kupeleka kiasi kilichosalia kwenye Fungu hili la maendeleo la Wizara hii ifikapo tarehe 30 Juni, 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchukua fursa hii kupongeza Wizara, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Bodi ya Korosho, Wakuu wa Wilaya zote za Mkoa wa Pwani na wadau wengine wa korosho kwa kuwezesha mfumo wa Stakabadhi Ghalani kuanza kutumika tena katika Mkoa wetu wa Pwani. Mfumo huu wa stakabadhi ghalani kwa mwaka huu umepelekea wakulima wa korosho wa Wilaya za Rufiji, Mkuranga, Kisarawe, Bagamoyo na Kibaha kupata bei nzuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia naipongeza sana Serikali kwa kuwezesha Vyama Vikuu na Vyama vya Ushirika vyenye madeni ya zamani katika Benki za CRDB na NMB kushiriki katika msimu huu wa korosho na kuweka utaratibu wa kurejesha madeni hayo ya Vyama vya Msingi bila kuathiri hela za wakulima. Naipongeza sana Benki Kuu ya Tanzania kwa kukubali kuwa msuluhishi/mpendekezaji wa utaratibu wa ulipaji wa madeni ya vyama hivyo bila kuathiri utaratibu wa Stakabadhi Ghalani.
Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Wizara kuhakikisha pembejeo za zao la korosho (dawa) zinapatikana kwa wakati ili kuongeza kiwango cha uzalishaji wa korosho na hivyo kuipelekea nchi kupata fedha za kigeni.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja hii.