Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Prof. Norman Adamson Sigalla King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. PROF. NORMAN A. S. KING: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Kwanza naishukuru Serikali ya CCM na Waziri wa Viwanda na Biashara kwa kazi kubwa waliyonayo mbele yao, lakini pia kwa kazi kubwa ambayo wanafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichangie tu kidogo, jambo tunalojadili ni muhimu sana kwa mustakabali wa nchi yetu; viwanda na biashara. Lakini duniani kote viwanda, biashara na uwekezaji ukiwemo ndani yake cha kwanza kabisa ni lazima mwekezaji awe anaamini kwamba wewe Serikali unamtazama yeye kama ni muhimu. Perception on investors lazima iwe very very positive.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa lugha rahisi ni kwamba lazima Mheshimiwa Mwijage rafiki yangu na wenzake wakiona watu wana fedha nyingi kwenye akaunti zao, wafurahie. Lazima wafurahie, ndiyo dunia ilivyo. Ni vizuri pia tufahamu mitego ya uchumi na biashara tunayosoma vyuoni na vile tunavyo-practice, mara nyingi havioani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii hata wewe mwenyewe ukiwa na shilingi trilioni moja, uka-deposit kwenye akaunti za US au Switzerland hakuna atakayekunyooshea mkono kwamba hii ni money laundering, lakini ukizitoa kwenye uchumi mkubwa ukazileta Tanzania, utaambiwa hela chafu. Nchi changa ni wajibu zijifunze juu ya mtizamo hii. Tukiweka fedha kwenye nchi zilizoendelea, hatuambiwi hela chafu, ukizitoa hizo hizo ulizoweka kwao, ukizileta Tanzania ni hela chafu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda pale Mexico wanalima dawa za kulevya, ukienda China wanalima dawa za kulevya, ukienda Afghanistan wanalima dawa za kulevya na ukienda Colombia wanalima dawa za kulevya. Wakubwa wa dunia hii huoni wanagombana na mataifa hayo juu ya dawa za kulevya. Nini tunajifunza? Maana yake uchumi na menejimenti ya uchumi na biashara duniani ni tricky, lazima ufikiri mara mbili kama unataka uwekezaji ukue.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naiomba sana Serikali kwa wawekezaji wenye fedha nyingi tuwaelekeze kwa kuwekeza, kwa sababu namna ya kupata fedha kwenye dunia hii ziko nyingi, ni ngumu hata kuzieleza. Siyo linearly, yaani ukichukua mtazamo wa linearity kwenye kutazama biashara, uta-fail kwa sababu biashara haiko hivyo, ina vitu vingi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wako watu hapa, tupo ambao msingi wa fedha zetu ni commission kwa sababu ni consultancy. Mzee Chenge pale Mwenyekiti yule, nguvu yake kubwa ni Mwanasheria mbobezi wa muda mrefu, kwa vyovyote vile anaheshimika ndani na nje ya Tanzania. Fedha zake za consultancy huwezi hata kuzitaja, lakini kama Mtanzania akijua kwamba akiweka fedha zake kwenye akaunti za Tanzania atahojiwa, hataweka, ataweka Kenya na kwingineko. Maana yake ni nini? Kutakuwa na homa ya uwekezaji na watu kuikimbia Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, chonde chonde namwomba rafiki yangu Mheshimiwa Mwijage, watu wakizileta fedha, tuhoji sana matumizi yake. Tukiona wameingiza fedha kutaka kuiangusha Serikali yetu, tuhoji. Ila fedha zikiingia, tuwaelekeze, wekeza kwenye minofu ya samaki, wekeza kwenye kiwanda hiki, wekeza kwenye kiwanda kile, ndiyo uchumi wa dunia ulivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichangie kidogo kuhusu Mchuchuma na Liganga. Chuma dunia nzima sasa uzalishwaji wake unapungua sana. China, Australia na USA ndiyo magwiji wa uzalishaji wa chuma. Mtaji tulionao wa chuma Liganga na Mchuchuma hakuna mradi; naomba niweke vizuri, hakuna mradi tulionao wa Tanzania leo ambao una uhakika wa fedha kwa maana ya kurudisha fedha kama Liganga na Mchuchuma. Bila kuuma maneno kabisa, hatuna project yoyote ya uwekezaji Tanzania ambayo inazidi mradi wa Liganga na Mchuchuma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwangu mimi naelewa hata ilipotengwa shilingi bilioni 13 kwa ajili ya compensation, who is going to be paid? Ni Mtanzania. Let them be paid. Nashangaa Wabunge wanahoji juu ya mtu wa Ludewa kulipwa fidia. Akilipwa mtu wa Ludewa, sana sana anawekeza Ludewa, Songea na Mwanza. Hakuna shida na hilo. You don’t upper the economy kwa ku-shift fedha kutoka BoT au Hazina kupeleka kwenye mifuko ya Mheshimiwa Mwijage anayowekeza Mwanza. Hakuna deterioration ya economy kwenye hilo. Is just good, ni jambo zuri kufanya hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba sana Liganga na Mchuchuma ipewe kipaumbele chake, lakini tukisema hivyo ndiyo maana tunasikia hadithi kwamba mafuta yamefika bandarini, I keep on wondering kwamba mtu anahoji kwamba point of origin hakuna documents. Serikali hupati chochote kwa declaration ya point of origin. Mwisho wa siku Mheshimiwa Mwijage wewe unachopata ni kodi. Kwa nini unauliza kama mafuta yametoka mbinguni au yametoka Kenya? Mafuta yameshafika bandarini, piga kodi, pata pato lako leta mafuta Tanzania. Simple as that. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unafahamu leo Tanzanite Kenya ni ya pili duniani, kwani Mheshimiwa Uhuru Kenyatta anahoji Tanzanite mnatoa wapi? Anauza, anapata kodi yake anaendelea na kujenga uchumi wake. India wanaongoza kwa kuuza Tanzanite, Rais na machinery ya India haihoji Tanzanite mnapata wapi? Siyo kazi yao. Ninyi pigeni kodi, leteni mafuta, kwa sababu sisi tunapata mafuta kwenye kodi, siyo kwenye documentation. Documentation hatusemi ni mbaya, zinakusaidia ku-facilitate upate kodi inayostahiki, siyo ikuzuie sasa kupata hata hela. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukishakalisha mafuta bandarini ni wazi yakija mtaani huku bei yake itakuwa kubwa. Kwa hiyo, tutazidi kuumiza wafanyabiashara na sisi wenyewe kujiumiza na Serikali kuiumiza. Kwa hiyo, lazima tuwe na correct perception jinsi ya kufanya tunavyoweza kufanya ili kuongeza uchumi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nampongeza sana Mheshimiwa Mwijage, niseme naomba sana aunde Kamati ya kumsaidia kwenye Wizara yake. Kamati ile siyo sisi, wafanyabiashara wamsaidie kufikiri namna bora ya kuwekeza. Mungu akubariki sana Mheshimiwa Mwijage. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.