Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante kwa kupata hizi dakika tano kuchangia Wizara hii ya viwanda. Kwa sababu mimi Liwale hakufikiki kwa barabara, hakufikiki kwa mawasiliano, hakuna umeme wa uhakika sitaongelea kuhusu viwanda ila nitajadili kitaifa zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumejadili sana namna ya kulinda viwanda vyetu kwa kulingana na ushindani usio sahihi. Lakini hatujajadili namna ya kulinda wafanyakazi wazawa. Tatizo la wazawa viwandani ni kubwa kuliko tunavyolifikiria, na mimi hapa ni-declare interest mimi hapa nimefanya kazi kwenye viwanda vya watu binafsi kwa miaka 25, kabla sijawa Mbunge. Kwa hiyo, ninachoongea hapa ninamaanisha. Nimefanya kazi kwenye viwanda kwa taaluma mimi ni msindikaji wa nafaka. Kwa hiyo, viwanda vyote vya nafaka hapa nchini nimefanya kazi, kwa hiyo ninachokisema namaanisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye nchi za wenzetu mwekezaji anapokuja kutoka nje anapewa limit ya wafanyakazi ambao anaweza kuwaajiri, lakini hapa kwetu ni utitiri. Mheshimiwa Waziri hata wafagizi kwenye viwanda vyetu hivi ni ma-expert. Hata madereva kutoa bidhaa kupeleka kwenye maduka ya jumla nima-expert, hata wasimamizi wa kupakia mizigo kwenye viwanda vyetu ni ma-expert. Kazi ambayo Watanzania wanaweza kufanya kwenye hivi viwanda ni ulinzi na ukuli peke yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili kama Taifa hatutaweza kuliangalia kwa upana wake tutaendelea kusema tunazalisha ajira, lakini ajira zenyewe ni ajira ambazo hazina mashiko. Tunasomesha wahasibu, storekeepers, tunasomesha Maafisa Utumishi lakini hawa wote hawawezi kupata kazi kwenye hizi sekta binafsi.

Pili, nataka niongelee suala la mazingira wezeshi ya uwekezaji. Mazingira ya uwekezaji Tanzania bado hayajawa sawa sawa na mfano mzuri nataka niwaambie kuna mfanyabiashara moja anaitwa Bakharesa alikuwa anataka kujenga grain terminal kwenye Bandari ya Dar es Salaam. Ili mchukua miezi sita kupata kibali, lakini tayari wakati anapata kibali alishakwenda Msumbiji na akapata na kwa nini alitaka kujenga Grain Terminal Dar es Salaam kwa sababu yeye ana viwanda karibu Afrika Mashariki nzima na Afrika ya Kati. Kwa hiyo akitaka kuitumia bandari ya Dar es Salaam kwa ajili ya kuagiza ngano zote kwa ajili ya viwanda vyake vilivyopo Barani Afrika. Lakini kwa sababu ya uzembe na urasimu sasa hivi Grain Terminal iko Msumbiji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, muone namna gani mazingira ya kweli yasivyokuwa rafiki kwa wawekezaji. Lakini sio hivyo tu katika nafasi hiyo hiyo wawekezaji labda hawa wa viwanda vikubwa tutawakosa nchi hii kwa sababu ya sera zetu. Leo hii mwekezaji aliyekuwa kwenye utawala wa Awamu ya Tatu ndio huyo huyo alikuwa fisadi kwenye Awamu ya Nne; mwekezaji aliyekuwa rafiki kwenye Awamu Nne ndio huyo huyo alikuwa fisadi kwenye Awamu ya Tano. Kwa maana hiyo Tanzania hatuaminiki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kwamba Chama cha Mapinduzi kinatawala tangu uhuru mpaka leo lakini kila tunavyobadilisha uongozi kwa maana ya Rais basi nchi hii inabadilika kama vile chama kilichotawala pale ni chama kingine. Kwa utaratibu huu hatutawezi kwenda kwa sababu hatuna mwelekeo. Hatuna goal moja ambayo kwamba kila atakaye kuja ataendeleza pale ambapo mwenzake ameacha. Kila Rais anayekuja anataka aanze moja. Hii ni sababu hakuna mwekezaji atakayekuja kuwekeza kiwanda cha miaka kumi. Maana yake tunahitaji viwanda, labda hizo cherehani kwamba kila baada ya miaka kumi Rais akibadilika mtu anafunga vyerehani vyake anaenda sehemu nyingine. Lakini kama tunakusudia kupata wawekezaji wakubwa lazima tujenge uaminifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile naomba niendelee kwenye page 185 ya kitabu cha Mheshimiwa Waziri. Mimi takwimu hizi kidogo zinanichanganya. Yaani wakati sekta ya viwanda mchango wake unaporomoka ndio sekta ya viwanda inakua, yaani sijui sijaelewa kuna majedwali pale yaani pato la Taifa mchango wa viwanda unapungua viwanda vyenyewe ndio vinapanda. Viwanda vikipanda mchango wa Taifa unashuka. Mheshimiwa Waziri mimi utakapokuja hebu uje kunieleza vizuri haya mambo yanakuwaje?

Mheshimiwa Mwenyekkiti, lakini jambo lingine lazima tukubali kwamba wawekezaji nchi hii wanaondoka kwa sababu ya sera zetu mbovu, kama hamkubali lakini lazima tukubali kwamba wafanyabiashara wakubwa wanahama nchi hii kwa sababu ya mazingira si sawasawa.