Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nakupongeza kwa kunipa fursa ya kuweza kujadili hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kiasi kikubwa napenda tu kuzungumzia suala la Mchuchuma na Liganga. Suala hili limekuwa likizungumzwa muda mrefu sana. Huu mfupa umekuwa mkubwa na mgumu. Liganga na Mchuchuma imeanza kuzungumzwa toka mwaka 1929 kipindi cha Mkoloni. Mkoloni alishindwa na hizi Serikali nyingine zote zimekuwa zinaweka mipango lakini ni mipango ambayo kwa kweli haitekelezeki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapozungumzia kitu kinachoitwa mradi ni lazima uwe na mwanzo na mwisho. Lazima kuwepo na activities au programs za kuhakikisha kwamba tunaanza hivi, tunapita hapa mpaka mwisho wa safari inakuwaje. Kitu kinachoshangaza katika Mradi wa Liganga na Mchuchuma ni kwamba hatuoni ile mipango ambayo inawekwa, kwamba sasa Liganga na Mchuchuma imewekwa kwenye Programu ya Miaka Mitano ya Serikali; Liganga na Mchuchuma imezungumzwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi; Liganga na Mchuchuma inawekwa kwenye kila bajeti ya mwaka ambazo tunazipitisha hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii ule Mpango wa Miaka Mitano sasa tunaingia mwaka wa tatu lakini bado hatujaona Liganga na Mchuchuma hasa ina tatizo gani. Tuliambiwa kwamba tatizo ni incentives, tunajaribu kujiuliza hizi incentives Serikali inashindwa kuchukua hatua ili tuweze kuona namna gani tunazi-accommodate na baada ya hapo hii miradi iweze kuanza? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimejaribu kupitia kitabu cha bajeti, nimeona Liganga imewekewa shilingi bilioni 5 na Mchuchuma imewekewa shilingi bilioni 5, lakini sasa haifafanui activity ya hizi shilingi bilioni 5 zilizowekwa kwenye Liganga na Mchuchuma ni kwa ajili ya nini hasa? Kwa hiyo, naamini kwamba Mheshimiwa Waziri atakapokuja kuhitimisha hotuba yake basi atatueleza hizi shilingi bilioni 5 ni kwa ajili ya nini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo ya fidia pale, mpaka leo imekuwa ni kizungumkuti. Alipita Mheshimiwa Waziri Mkuu tarehe 26 Januari, 2017, tulilizungumzia kwa kiasi kikubwa suala la fidia na ikaonekana kama fidia imekuwa exaggerated na ikasemekana kwamba itaweza kuundwa Tume au tukafanya review ya ile fidia ili wale watu waliopisha ile miradi iweze kufanyika pale walipwe kwa sababu sasa hivi wala hawajui nini cha kufanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye incentives kule tunaona kuna suala la Power Purchase Agreement. Mara ya kwanza ilikuwa ungetumia ule mfumo wa Build, Own and Transfer lakini baadaye kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri ya mwaka 2017, wakaja tena na mfumo ule mwingine kwa maana ya kubadilisha kwamba itakuwa ni Build, Own and Transfer. Sasa hatujajua ni incentives zipi ambazo zinasababisha ule mradi usianze? Kwa hiyo, naamini Mheshimiwa Waziri atakapokuja basi atatuambia wamefikia wapi. Hizo incentives ambazo zinasemwa kwamba zinashindikana kufanya ule mradi uanze ni zipi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza kwamba kuna miundombinu wezeshi ambayo inafanya sasa ule mradi unaweza ukaanza, lakini pia inahitaji maamuzi magumu. Naona upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ambazo zinakwenda kwenye ile miradi, kwa maana kuna barabara inayotoka Mchuchuma kwenda Liganga na pia kuna barabara ambayo inatoka Mkiu kupitia Liganga kwenda Madaba. Naona zoezi lile linakwenda vizuri na upembuzi yakinifu na usanifu wa kina safari hii utaisha mwezi Oktoba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaona umeme wa Gridi ya Taifa ambao vilevile utashushwa pale eneo la Liganga na pia moja kwa moja utaelekea kule Mchuchuma. Jitihada hizi za Serikali tunaziona, miundombinu wezeshi hii ya Serikali tunaiona. Napenda kuiomba Serikali, suala la fidia basi mwaka huu iwe mwisho. Wale watu wamesubiri kwa muda mrefu, tuondokane nalo hilo. Kama itashindikana mwekezaji kulipa basi Serikali ichukue jukumu hilo na kuhakikisha kwamba hii adha ya fidia kwa wananchi wetu wa Mkomang’ombe na kule Mundindi inaisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mchuchuma na Liganga tumekuwa tukiiongelea muda mrefu sana. Mimi na watangulizi wangu wote nane wamekuwa wakiongelea Mchuchuma na Liganga katika Bunge lako hili. Mwaka 2017 zaidi ya asilimia 80 ya Waheshimiwa Wabunge wamekuwa wakiiongelea Mchuchuma na Liganga. Tukijaribu kuangalia kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri, Mchuchuma na Liganga haijapewa ile weight yake yaani ni maneno ya mistari 11 tu, basi Liganga na Mchuchuma imeisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ikumbukwe tunasema kwamba Liganga na Mchuchuma ni miradi kielelezo. Miradi kielelezo ya nchi sikutegemea kwamba ingeweza kupewa weight ndogo kiasi hiki. Tungeweka weight kubwa na tujue tatizo ni nini? Angedadavua kiasi cha kutosha ili Waheshimiwa Wabunge tujengewe uelewa ili mwisho wa siku tuweze kuishauri Serikali vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nanukuu maelezo ya Mheshimiwa Waziri ya masuala ya viwanda mama na miradi kielelezo ya nchi, Mradi wa Mchuchuma na Liganga. Anasema, katika kufanikisha utekelezaji wa Mradi Unganishi wa Mchuchuma na Liganga, Serikali iliunda Timu ya Wataalam wa Serikali ikiwa na jukumu la kuchambua vivutio vilivyoombwa na wawekezaji. Vilevile uchambuzi ulifanyika kwa kuzingatia marekebisho ya Sheria ya Madini, 2010; Sheria ya The Natural Wealth and Resources Permanent Sovereignity Act, 2017; na The Natural Wealth and Resources Contracts (Review and Renegotiation of Unconscionable Terms), 2017 na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa na Serikali. Timu hiyo imekamilisha taarifa ya awali ambayo inasubiri kutolewa maamuzi na mamlaka husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maelezo haya ni ya kila siku na kwenye kila bajeti huwa yanakuja haya haya, kwamba tunaendelea na mchakato. Sasa ifike wakati Serikali ije na maamuzi magumu kuhusu mradi huu. Kwa hiyo, bado Taifa linasimama na naamini kwamba unapozungumzia viwanda ndani ya nchi hii, unazungumzia Liganga na Mchuchuma kwa sababu multiplier effect yake inaenda mbali. Kwa hiyo, ifike mahali sasa tuchukue maamuzi magumu. Nami naamini kwamba Serikali ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ina uwezo wa kuchukua maamuzi magumu na kuhakikisha kwamba miradi hii ina-take-off. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye upande wa biashara, mimi huwa najiuliza, tunawajua wafanyabiashara wetu? Tunayo database ya wafanyabiashara wetu? Kwa sababu tunaweza tukawa tunazungumza biashara na inaweza ikaleta impact gani wakati hatuwafahamu wafanyabiashara wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama mlivyo-categorize, kuna wafanyabiashara wa kati, wadogo na wakubwa. Je, tunayo hiyo database ya hao watu kiasi ambacho tunaweza tukawa na uhakika kabisa kwamba tunapozungumzia suala la biashara impact yake ni hii na revenue tutakayoipata kwa wafanyabiashara ni hii hapa ili mwisho wa siku sasa tutengeneze platform kwenye kila maeneo, tunaweza tukaweka semina kwa wafanyabiashara wa kati, wadogo na wakubwa. Otherwise tutatakuwa tunatwanga maji kwenye kinu kama hatuwajui wafanyabiashara wetu ni nani na tunatarajia nini kutoka kwao na impact kwa wananchi wetu kiuchumi kuanzia mtu mmojammoja, vikundi na mpaka Taifa inakuaje?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ifike mahali sasa hawa Maafisa Biashara wetu kwenye Halmashauri, kwenye mikoa, ni lazima watengeneze database za wafanyabiashara wetu. Kwa sababu database hiyo inaweza ikatumika kama role model kwa watu ambao wanataka kuingia kwenye biashara ili waweze kujua kwenye biashara playground yao ikoje? Sometimes tukiwa na role models wana uwezo wa kushawishi watu wengine kuja kuingia kwenye mfumo wa kibiashara. Tusipotengeneza semina hizi wezeshi hatutaweza…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naunga mkono hoja.