Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Hassanali Mohamedali Ibrahim

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiembesamaki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. IBRAHIM HASSANALI MOHAMMEDALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Namshukuru Mwenyezi Mungu vilevile kwa kunipa uzima wa afya nikiwa nimesimama hapa kwa nguvu zake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze kaka yangu Waziri wa Biashara na Viwanda, Mheshimiwa Mwijage. Kwa kweli, hiki kitabu nimekipitia leo mchana vizuri kabisa, nakiona kipo vizuri sana. Nimpongeze yeye na timu yake nzima kwa jinsi walivyoandaa bajeti hii na ripoti ya Wizara ya Biashara na Viwanda, Mheshimiwa Mwijage na timu yako hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nichukue nafasi hii nimshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa mambo aliyoyaweka jana vizuri sana. Amewatoa wananchi wasiwasi, maneno yalikuwa mengi kwamba katika Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan kutakuwa hakuna mafuta na sukari. Tunamshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu pamoja na Mheshimiwa Mwijage kwa kutuhakikishia kwamba, hakutakuwa na suala hilo wala matatizo hayo ya mafuta wala sukari. Nawashukuru sana Mheshimiwa Waziri Mkuu na Mheshimiwa Mwijage. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitakuwa mwizi wa fadhila kama sijampongeza Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli kwa jinsi anavyohangaika kufufua viwanda ambavyo vilikuwa vimekufa. Naweze kusema kwamba jitihada ya Mheshimiwa Rais imetuletea faraja kubwa sana na naamini kwa Waziri aliyekuwa naye ni Waziri jembe kabisa, Mheshimiwa Mwijage. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mwijage nimefanya naye kazi wakati nilipokuwa kwenye Kamati ya Biashara na Viwanda miaka miwili iliyopita. Namjua kazi yake, ni mtu ambaye yuko straight kabisa na makini kabisa, hongera sana Mheshimiwa Waziri kwa hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nilikuwa na ushauri kwa Wizara ya Biashara na Viwanda. Mheshimiwa Mwijage nataka utusaidie au uwasaidie wafanyabiashara ambao wanapakia mizigo yao Dubai kuja Dar-es-Salaam wanalipia SGS kule Dubai na kila item wanatozwa kwa Dola 20 mpaka Dola 30. Baada ya ku-register SGS Dubai wanatakiwa baada ya mali kufika hapa TBS inawa-charge tena katika kuchunguza vile vitu walivyoleta. Kwa hiyo, wanakuwa wanalipa SGS kule Dubai wakija huku wanachajiwa tena na TBS. Sasa utakuta mfanyabiashara analipa mara mbili ya kile kitu ambacho amekinunua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu wa SGS kule Dubai wamekuwa very slow yaani ukiwapelekea sampuli, huchukua more than four or five weeks, sasa utakuta mfanyabiashara anaumia na kule ameweka mzigo kwenye godown za watu analipa zile gharama kwa sababu Dubai hakuna mtu ambaye atakuwezesha kukuwekea mali kwa mwezi mmoja, mwezi mmoja na nusu. Kwa hiyo, nashauri Mheshimiwa Waziri labda ukae na hawa wenzetu wa SGS Dubai na TBS, kwa nini wanakuwa wana-charge mara mbili mzigo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine kwa sababu, tukiwasaidia wafanyabiashara naamini watapata nguvu ya kutuletea mali kwa wingi na Wizara ya Fedha itapata kodi. Kwa hiyo, hapa tunampa motisha mfanyabiashara at the same time Wizara ya Fedha na TRA wanapata pesa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kuna tatizo moja kubwa la wenzetu hawa wa TFDA. Naweza kusema kwamba TFDA sio wote, sitaki kuwakaanga wote, baadhi yao hupelekewa sampuli ikiwa ya maziwa, juice au kitu chochote wanakwambia kwamba utapata ripoti after 60 or 70 days. Mheshimiwa Mwijage wenzetu hawa TFDA hivi kweli wanatutakia mema Tanzania hii? Wakati wewe unapigania wafanyabiashara walete mali wauze nchi ipate pesa tupate kodi, wanaambiwa warudi after 70 days?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi navyozungumza haya huwa nina ushahidi, sizungumzi tu kwa kuwaelemea TFDA. Kwa hiyo, naomba TFDA kama kuna upungufu wa watu basi waajiriwe watu wengine lakini huwezi kumuweka mtu 60 or 70 days ndiyo unampa report, inarejesha nyuma maendeleo yetu na sisi tunataka kusonga mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu hata hizo ada ambazo wana-charge TFDA ni kubwa sana Mheshimiwa Waziri. Ningeomba kidogo hizo ada ziteremshwe ili watu wawe na hamu ya kuleta mali nchini. Kiwango kinachotozwa sasa hivi ni kubwa sana. Hata hivyo vitu ambavyo SGS wana- charge kule Dubai kwa kila item ni Dola 30 nyingi Mheshimiwa Mwijage. Wewe ni msikivu naamini utachukua hatua. Haya ndio yalikuwa ni kero na nilikuwa natoa ushauri kupitia Wizara yako ifuatilie kwa karibu sana hili suala ili tufike hapo tunapotaka kwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashangaa sana watu wanapoiponda Serikali hii, mimi siwafahamu. Kwa sababu, hiki kitabu kimeeleza kuna wawekezaji 99 wamesajili kuanzisha viwanda Tanzania hii. Ina maana hao wawekezaji ambao wanakuja kuwekeza hapa si wendawazimu, wameshajua Tanzania ni nchi ya amani, Tanzania kuna kuna moja, mbili, tatu. Sasa wanapoponda kwamba hakuna viwanda au hakuna chochote wasome hiki kitabu ambacho kimeandikwa kwenye ukurasa wa 186, miradi mipya ya viwanda vilivyosajiliwa na TIC mwaka 2017/2018. Hii ni ushahidi tosha kwamba watu wana imani na Serikali ya Mheshimiwa Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kuna wengine wanakuwa na choyo na binadamu sisi tunakuwa na choyo. Mheshimiwa Mwijage ukivaa suti nzuri kama mtu hakupendi atakwambia unaringa lakini kwa sababu umevaa suti nzuri. Kwa hiyo, nasema tupunguze uchoyo, tumpe haki yake Mheshimiwa Rais Magufuli anavyofanya hii kazi kwa sababu, kuileta Tanzania katika amani ni kitu kikubwa sana ndio maana hawa wawekezaji 99 wamekuja kuwekeza Tanzania billions of Dollars, it is billions of Dollars. Leo kwa nini tunakaa tunaiponda hii Serikali? Why? Badala ya kuipa nguvu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini katika miaka michache ijayo tutakwenda kwenye uchumi wa kati, hapa tulipo tutasonga mbele. Ni juhudi zetu sisi Watanzania, Wabunge waliokuwa humu ndani tumpe nguvu na ushirikiano Mheshimiwa Rais pamoja na Mawaziri wake wote walikuwa humu ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wanaposema kwamba labda kiwanda kiwe na ekari tano, ekari sita, kule China unaweza kukuta kichumba kidogo sana wanazalisha mambo ambayo huwezi kuyaamini Mheshimiwa Mwijage. Wana vyerehani 10, 15 lakini the production ambayo wana- make ni kubwa sana. Kwa hiyo, kiwanda si lazima kiwe na ekari 10 ndiyo ukaita kiwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana na naipongeza sana Wizara hii na naiunga mkono asilimia 100 Wizara ya Biashara na Viwanda. Inshallah Mwenyezi Mungu atatusaidia na tumuombee Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, ahsanteni sana.