Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutumia nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote kwa kazi kubwa wanayofanya Wizara hii. Hongereni sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na pongezi hizo, naomba kuelezea shida na adha kubwa ya ukosefu wa maji safi na salama katika Jimbo la Kwela.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na adha hiyo, tunaomba Serikali itupatie fedha za kutekeleza miradi ya maji kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji Muze Group kwa vijiji vifuatavyo ambavyo vinaweza kupata maji katika chanzo cha maji cha Mto Kalumbaleza ni Kalumbeleza, Mnazi (MUA), Mnazi Mmoja (ASILIA), Ilanga, Mbwilo, Muze, Kalakala, Uzia, Isangwa na Kalumbale (B).

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kuna Mradi wa Maji wa Kifinga kwa vijiji vya Kifinga na Mkamba; na Mradi wa Maji wa Mtowisa ambao unatakiwa kufanyiwa ukarabati na kupanuliwa kwa kuhudumia vijiji vya Mwela, Mtowisa A, Mtowisa B, Lwanji, Ng’ongo na Sontaukia.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia upo mradi wa maji wa kijiji cha Msia na Mradi wa Ilemba unaotakiwa kufanyiwa ukarabati kwa kupanuliwa na kufikia vijiji vyote vya Ilemba A, B, C na Kaswepa.

Mheshimiwa Naibu Spika, upo Mradi wa Maji wa Kaoze Group utakaosaidia vijiji vya Kaoze, Kianda Igonda, Mazinge na Kitongoji cha Kikwale.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna Mradi wa Kaesenga Group kwa vijiji vya Kaengesa A, Kaengesa B, Mkunda, Itela, Kitete, Kazi na Kazi Katonto. Vilevile tunao Mradi wa Kijiji cha Lyapona.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo Jimbo langu lina mabonde makubwa na mito mingi inayofaa kwa miradi ya umwagiliaji. Nashangaa kuona Wizara haijatenga fedha za umwagiliaji katika Jimbo langu kwa miradi ifuatayo:-

(1) Mradi wa Umwagiliaji wa Maleza hekta 7000;
(2) Mradi wa Maji wa Umwagiliaji wa Nkwilo;
(3) Mradi wa umwagiliaji wa Uzia;
(4) Mradi wa Umwagiliaji wa Msia;
(5) Mradi wa Umwagiliaji wa Milepa; na
(6) Mradi wa Umwagiliaji wa Ilemba.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba kutoa ushauri kwa miradi ya maji inayojengwa nchini baada ya kumalizika, itengewe fedha za matengenezo (service) kuliko kutegemea michango kuliko kutegemea michango ya wananchi ya shilingi 50 kwa ndoo moja. Kiasi hicho ni kidogo sana, hakiwezi kutosha kutengeneza miradi mikubwa ya maji iliyotumia mabilioni ya fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho naunga mkono hoja. Ahsante.