Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na Bonde la Mto Ruhuhu; mwaka 2016/2017 kuliwekwa lengo la ujenzi wa bwawa la umwagiliaji katika Bonde la Mto Ruhuhu ambalo linalounganisha Wilaya za Ludewa na Nyasa. Cha kushangaza bajeti ya mwaka 2017/2018 na mwaka 2018/2019 haijawekwa kabisa. Sasa ningeomba Serikali inipe ufafanuzi kuna tatizo gani lililotokea mpaka likaondolewa kwa mwaka 2017/2018 na 2018/2019 na hata kwa mwaka uliowekwa tengo hakuna kinachoendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Bonde la Umwagiliaji Lifua, tunaishukuru Serikali kwa kutupatia fedha kwa ajili ya Skimu ya Umwagiliaji ya Lifua ambayo kilimo cha mpunga kinastawi sana. Skimu hiyo imekamilika kwa asilimia 75. Tungeomba sasa Serikali itupe asilimia 25 zilizobaki ili tukamilishe kwa kiasi cha asilimia 100.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa uchimbaji wa visima katika vijiji vya Tarafa ya Masasi, kufuatia uwekwaji wa umeme wa REA katika vijiji vya Tarafa ya Masasi yaani Iwela, Kimetembe, Nkomang’ombe, Luilo, Lifua, Kipangala, Kingole, Lihagule, Kiyogo, Manda, Igalu, Mbongo, Ilela, Ngelenge, Kipingu na Kipangala, tukichimba visima hivyo walau vitatu kila kijiji nina imani kwa kushirikiana na wananchi, tutatatua tatizo la maji kwa asilimia kubwa katika tarafa hii. Nina imani tukiweka mpango kazi tatizo hili litaisha katika maeneo haya ambayo water table ipo jirani sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu miradi ya maji katika Wilaya ya Ludewa; kumekuwa na tatizo kubwa kwa wakandarasi wengi wa maji kutolipwa mapema pindi wanapowasilisha certificates zao Wizarani kwa malipo ili kazi iendelee. Inachukua muda mrefu sana toka wawasilishe certificates na malipo jambo linalopelekea miradi mingi kuchelewa na kukwama. Hii inapelekea hata lengo la pesa iliyo katika bajeti kubaki huku miradi ikiwa bado haijamilika. Kuna haja ya kuangalia namna nzuri ya malipo na ikiwezekana tutumie mfumo wa force account ambao umeleta ufanisi mkubwa katika miradi ya ujenzi hasa wa vituo vya afya.