Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa dhamira yake ya dhati kuhakikisha Serikali yake inamtua ndoo kichwani mama wa Kitanzania mijini na vijijini.

Mheshimiwa Naibu Spika, nawapongeza pia Mheshimiwa Waziri wa Maji na Naibu wake, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Wakurugenzi na watendaji wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchangia kwenye Wizara hii ya Maji kama ifuatavyo; maji ni uhai, maji ni roho, maji ni utu, yaana zaidi ya 65% ya mwili wa binadamu na maisha ya wanyama, mimea na binadamu yanategemea maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndani ya Jimbo langu la Busokelo kuna miradi ya maji ambayo inaitwa Mwakaleli I tangu mwaka 2009 hadi leo hii mradi huu bado haujakamilika na mkandarasi anasuasua kiasi kwamba hadi sasa chanzo cha maji hakijajengwa na wananchi wangu wanapata shida kubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto kubwa kwenye Wizara hii ni ukosefu wa wataalam ngazi za Halmashauri na Mikoani inayosababisha miradi mingi kushindwa kuendelea na kusimama. Wataalam wa Halmashauri wapo chini ya Wizara ya TAMISEMI, lakini Wizara ya Maji ambao ndiyo wasimamiaji wakuu wa maji, hawana mamlaka juu ya wataalam hao Halmashauri na hivyo kupelekea kuwa vigumu kuwawajibisha wanapokuwa wamekosea. Ushauri wangu wataalam hawa wawe chini ya Wizara ya Maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja ya kuanzishwa kwa Wakala wa Maji Vijijini ili waweze kusimamia kwa ukaribu na ufasaha kuliko hivi ilivyo kwa sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la miradi ya umwagiliaji limekuwa ni tatizo kubwa sana kwa wananchi wa Jimbo la Busokelo. Kuna skimu za umwagiliaji kwenye Mto Mbaka, Kata ya Kambasegela imesahaulika na kuna kituo cha umwagiliaji ambacho kilijengwa tangu mwaka 2009 hadi sasa hakuna mwendelezo wa aina yoyote na hivyo kuisababishia hasara Serikali maana kuna majengo ambayo tayari yalijengwa kama nyumba ya mtumishi, madarasa, mabweni ila bado bwalo tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja ya kuongeza shilingi 50 kwa lita moja ya mafuta aina ya dizeli ama petroli.

Mheshimiwa Naibu Spika, wataalam wetu ngazi za Halmashauri ni muhimu wapewe/kuwezeshwa namna ya ku- design na ku-survey miradi ili zoezi hili lisitegemee wataalam toka Wizarani.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.