Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, nitoe shukrani kwa ujenzi wa miradi miwili iliyosimamiwa na MUWASA katika Jimbo la Moshi Vijijini, ule wa Mang’ana ulionufaisha vijiji vya kata ya Uru Kusini na Uru Kaskazini na ule wa Kaloleni unaonufanisha vijiji vya kata ya Mabogini.

Mheshimiwa Naibu Spika, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji aliahidi kupanua miradi ya MUWASA ili vijiji vilivyobaki katika kata ya Mabogini viweze kunufaika vyote yaani Mtakuja, Msarekia, Muungano na Remiti. Aidha, kata ya Kimochi sehemu kubwa ya miundombinu ya maji ni ya miaka mingi sana na imechakaa sana, inahitaji ukarabati na mahali pengi kujengwa upya. Tunahitaji Serikali kuja kufanya tathmini na kuchukua hatua.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa Mbokumu unaohudumia vijiji vya Tema, Kiwalaa na Korini Kusini na Kaskazini umekamilika lakini kuna malalamiko mengi sana juu ya kiwango cha ubora wa kujengwa kwake. Naomba Wizara ije ione ukweli huu na kuchukua hatua kwa kuwa mradi huu haufanyi kazi vizuri. Maji mengi bado yanapotea njiani na virura vingi havitoi maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho tunahitaji Wizara kuonesha kuunga mkono mifereji yetu ya asili katika vijiji vyetu vyote vya Moshi Vijijini kwani mingi inahitaji ukarabati mkubwa kidogo ambao wananchi wenyewe hawawezi.