Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu naomba kuhoji Serikali kimaandishi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa maji taka Mtwara Mjini upoje, Mtwara Mjini hakuna mfumo wa maji taka kabisa na bahari ipo karibu kabisa. Nataka kujua kwa nini Serikali haitaki kujenga mfumo wa maji taka Mtwara Mjini? Kuna uchafu mwingi sana majumbani ambao kungekuwa na mfumo wa maji taka magonjwa kama kipindupindu yasingeweza kutokea Mtwara Mjini.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukosefu wa maji taka Dodoma - Chaduru; Dodoma Jijini Mtaa wa Medeli Mashariki eneo la Chaduru hakuna mfumo wa maji taka. Wabunge wengi tunaishi huko, ni karibu na Bunge, ni mjini sana lakini hakuna mfumo wa maji taka. Je, ni lini mfumo huo utafika Dodoma Chaduru?

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi ya maji Mtwara Mjini kusuasua, naongea tena, miradi ya maji Mtwara Mjini inasuasua sana. Mkandarasi wa mradi wa kutoa maji Lwelu kuja Mitengo, Mbae na Ufukoni anasuasua kwa sababu hapati fedha kwa wakati. Naomba kujua kwa kuwa pump test tayari imefanyika lini ataanza kuchimba matenki na kusambaza maji kwenye kata husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, fedha za maji Mtwara Mjini haziji, ukurasa wa 224 wa hotuba ya Waziri wa Wizara ya Maji ametaja maeneo ya Mkoa wa Mtwara ambapo pesa zimepelekwa kwa ajili ya miradi ya maji, cha kushangaza Mtwara Mjini (Manispaa) hakuna hata senti moja iliyopelekwa. Naomba kujua kwa nini wananchi wa Mtwara Mjini hatupewi pesa za Serikali kwa ajili ya maji?