Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na Mradi wa Maji Mjini Nansio. Bado mradi huu haujaweza kuwa na tija kufikia malengo yaliyotarajiwa kuondoa tatizo la maji kwa wananchi zaidi ya 70,000 katika Mji wa Nansio. Hili linatokokana na matatizo ya mara kwa mara kwenye mfumo wa mradi huu. Mfano, kupasuka kwa mabomba na wakati mwingine kukatwa kwa umeme kwenye mtambo wa kusukuma maji, kutopanuliwa kwa mtandao wa mabomba na kadhalika. Hali hii imekuwa inachangia kuendelea kwa maradhi mengi yanayosababishwa na matumizi ya maji yasiyokuwa safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri/ombi, Mamlaka ya Maji Mwanza (MWANAUSA) iweze kusimamia na kufuatilia kwa karibu ili kuondoa tatizo la maji katika Mji wa Nansio.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa maji vijijini (vijiji kumi) kutokamilika kwa haraka kwa mradi huu ni kikwazo kwa upatikanaji wa maji salama katika vijiji mbalimbali katika Wilaya ya Ukerewe. Hii inasababishwa pamoja na sababu nyingine kutokuwa na watumishi wa kutosha wenye utaalam katika fani ya maji mfano, wahandisi, mafundi mchundo na kadhalika. Ombi/ushauri wangu ni moja, Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ipatiwe wataalam wa kutosha katika Idara ya Maji. Mbili, wakandarasi wanaohusika katika usambazaji maji wafuatiliwe kwa karibu kupitia Mhandisi wa Maji Wilayani kulipwa kwa wakati ili mradi huu ukamilike kwa wakati/haraka na kutoa huduma kwa wananchi wengi kadri iwezekanavyo.