Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Segerea linakabiliwa sana na uharibifu wa miundombinu ya barabara inayosababishwa na kupasuka mabomba ya maji mara kwa mara. Je, ni kwa nini Wizara haisimamii yakanunuliwa mabomba yenye viwango kuepusha hasara ya uharibifu wa miundombinu hiyo? Mfano, barabara ya Mnyamani, Kata ya Vingunguti, Kata ya Kisukuru, Kata ya Tabata barabara ya Mawenzi – Mwananchi, Kata ya Kimanga, barabara ya Twiga, barabara ya Kimanga Liwiti; kupitia mtaa wa Amani, barabara ya Bombom Kijiwe Samri Kata ya Minanzi Mirefu na Kiwalani.

Mheshimiwa Naibu Spika, usafishaji wa mabwawa ya Spenko yanayotumika kuhifadhi maji taka toka viwanda katika eneo la Mnyamani, Mtaa wa Mji Mpya na Kisiwani. Ni lini haya mabwawa yatakumbukwa kwa kuwa yanatoa harufu mbaya kwa wakazi wa eneo hili?

Mheshimiwa Naibu Spika, kisima cha maji safi kimeendelea kukamilika katika Kata ya Kisukuru, ni ombi letu kwamba vifaa vya usambazaji maji vifike kwa wakati hasa mabomba ya mradi katika eneo hili la shule ya msingi Magoza ambapo pia Naibu Waziri alifika.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kusisitiza umuhimu wa kuanzisha kilimo cha umwagiliaji hasa wa mboga mboga katika maeneo ya Chanika ili kuondosha tatizo la wananchi kula mboga zenye sumu zinazolimwa Mto Msimbazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni muhimu Wizara ije na mpango wa namna gani itazidi kudhibiti upotevu wa maji yanayovuja mitaani ilhali maeneo mengine hayapati maji kama vile upotevu wa maji BAWASA wa thamani ya shilingi bilioni 1.5.

Mheshimiwa Naibu Spika, CAG ameainisha kiasi kikubwa cha pesa kinakusanywa kupitia kwa Wakala wa MAXCOM kutowasilishwa kwa wakati licha ya kwamba inakuwa imekusanywa kiwango hicho kwa niaba ya TANESCO, mfano mpaka Juni, 2017 MAXCOM alikusanya shilingi milioni 756 na aliwasilisha shilingi milioni 400 tu. Hii inaathiri utendaji wa DAWASCO na kuendelea kukwamisha juhudi za maji Mkoa wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, DAWASCO imeelezwa kutumia isivyo fedha zilizotengwa kufanikisha uunganishaji wa maji kwa wateja wapya kwa mujibu wa CAG page 84 report ya ukaguzi wa mashirika ya umma kwa mwaka 2016/2017.