Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Katibu Mkuu wa Wizara kwa kazi nzuri. Ninayo maeneo ambayo ningependa niyasemee.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukosefu wa maji safi na salama katika Wilaya ya Kigamboni, Wilaya hii hakuna utaratibu wa upatikanaji wa maji na mfumo wa utoaji wa maji taka. Eneo la Mbagala pamoja na jitihada za Serikali kuchimba visima virefu Mbagala na kusambaza maji lakini bado hatujafikia asilimia 100. Maeneo ya Chamazi, Mbande, Toangoma, Kibondemaji, Mchikichini na Mianzini hata visima vyenyewe ni vya shida.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu visima vya Kimbiji na Mpera, napongeza sana Serikali kwa kuchimba visima, vimekamilika kwa asilimia kubwa. Swali langu kama visima karibu saba vimekamilika kwa nini hakuna utaratibu wa kuanza sasa kusambaza maji angalau kwa kata zilizo jirani na visima hivyo? Kata ya Kisarawe II - Kibada, Pemba Mnazi na zile zilizo jirani tuanze kutumia maji ya visima hivyo?

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mfumo wa maji taka, kwa kweli kuna tatizo la maji taka Kurasini, maeneo hayo yamekuwa ya mjini na mifumo imekuwa ya kizamani. Ni vema tukaangalia vizuri mfumo mzima wa maji taka Wilaya za Temeke, Kigamboni, Ubungo na Kinondoni. Ilala kuna nafuu kidogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Bwawa la Kidunda; Serikali iangalie na waweke fedha katika Bwawa la Kidunda kusaidia upatikanaji wa maji kwa uhakika katika Mto Ruvu. Wakazi wa Dar es Salaam tunategemea sana Bwawa la Kidunda kupata maji safi ya kunywa toka Mto Ruvu, lakini kipindi cha kiangazi maji yanapungua, kwa hiyo tunahitaji hilo bwawa lijengwe ili lisaidie.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja asilimia mia moja.