Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Wizara ikiongozwa na Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote kwa kazi wanayofanya na kuweza kutekeleza zaidi ya asilimia 50. Lini mradi wa maji toka Ruvu Juu kwenda Kisarawe utaanza ukizingatia kazi zote muhimu za uzalishaji mradi huo umeanza, wananchi wanahitaji maji na viwanda pia vinahitaji maji. Mradi wa Kimbiji na Mpera lini utaanza?

Mheshimiwa Naibu Spika, Mto Wami una maji mengi sana lakini wakati wa mvua maji hayo huwa machafu, nini mpango wa Serikali wa kuweza kuyasafisha yatumike wakati wote na kuweza kuondoa kero za wananchi Mkoa wa Pwani. Nini mkakati wa Serikali kwenye matumizi ya maji ya Mto Rufiji? DAWASA wapewe jukumu la kuvuna maji ya mvua maeneo ya shule na hospitali. Naunga mkono hoja.