Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Naibu Spika, nipende kuchangia na kuzungumzia yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu miradi kujengwa chini ya kiwango; miradi mingi nchini inajengwa chini ya kiwango hivyo kutumia fedha nyingi za Serikali na kuleta hasara kwa Serikali, huku ikiachwa miradi hiyo itakuwa haitoi maji kama ilivyotegemewa. Mfano, Mradi wa Maji wa Vikawe wenye gharama ya shilingi milioni 531 ambao hautoi maji baada ya wananchi kuukataa kutokana na mabomba kuvuja na kuongeza gharama za maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu umwagikaji maji hovyo (upotevu wa maji), nashauri Serikali kuliangalia suala hili la maji kwa wananchi imekuwa kawaida kwa mamlaka kurudisha hasara kwa wananchi. Mamlaka zimekuwa zikifanya uzembe wa kufanya matengenezo ya mara kwa mara ili kudhibiti upotevu wa maji unaondelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, uhaba wa wahandisi wa maji, maeneo mengi hapa nchini hakuna wahandisi wa maji, wanatumiwa wale ambao hawana ujuzi na hivyo kusababisha miradi mingi kujengwa chini ya kiwango. Mfano, Mhandisi wa Halmashauri ya Kibaha ambaye ni wa mazingira hivyo kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi. Naishauri Serikali kuendelea kuwaandaa wahandisi katika vyuo vyetu ili kupata wahandisi bora ili kulinda fedha za Serikali zinazopotea bila sababu.