Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na uchakavu miundombinu. Kulingana na miradi mingi ya umwagiliaji kutekelezwa ikiwa chini ya kiwango na kuleta usumbufu mkubwa kwa wananchi na kuwa chanzo cha upotevu wa pesa za wananchi wanaolipa kodi halafu zinaliwa na watu wachache ambao Serikali iwachukulie hatua za kinidhamu wale wote waliochukua na kutumia pesa za walipa kodi wa nchi hii.

Miundombinu ya maji imekuwa changamoto kubwa na kusababisha upotevu mkubwa wa maji pale ambapo inatokea mabomba kupasuka na kusababisha upotevu mkubwa wa maji katika maeneo mbalimbali nchini. Serikali inapaswa kulitafutia ufumbuzi ili kumaliza suala hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, taasisi nyingi kuendelea kudaiwa na kusababisha maumivu makali kwa Watanzania ambapo wanaotakiwa kulipa ni Serikali. Inapochelewa kulipa madeni hayo kwani kunakuwa na ubaguzi kwani wananchi wa kawaida wasipolipa bili japo ya mwezi mmoja wanakatiwa maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kutumia Ziwa Tanganyika hususan kusambaza maji katika mikoa inayozunguka Ziwa Tanganyika, suala hili likikamilika litasaidia kumaliza changamoto zinazokabili mikoa ya Rukwa, Kigoma, Katavi kwani wananchi wakitumia ziwa hilo ambalo litakuwa la uhakika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu bili hewa, kumekuwa na utaratibu mbovu sana wa bili za maji kuja wakati maji hayatoki. Hizi mita zinakuwa na shida au watu wote walipe madeni ambayo ni halali.