Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ZITTO R. Z. KABWE: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya CCM, zililongwa mbali, zilitendwa mbali. Katibu Mkuu Hazina na sekta binafsi kushiriki kwenye sekta ya maji kinyume na sera ya Serikali na kauli ya Wizara ya Maji. Kiburi anapewa nani?

“Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kuwepo kwa mahitaji makubwa ya kuboresha huduma za maji na umwagiliaji, mchango wa sekta binafsi kwenye uwekezaji katika kutoka huduma hizo bado si wa kuridhisha. Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuhamasisha ushiriki wa sekta binafsi, ikiwa ni pamoja na kutunga Sera ya Taifa ya Ubia baina ya Sekta ya Umma, Sekta Binafsi ya mwaka 2009 na Sheria ya Ubia ya mwaka 2010 na Kanuni zake ili kuweka mazingira mazuri ya kuwavutia wawekezaji. Vilevile Wizara imeendelea kuwapatia wataalam wake mafunzo yanayohusu uwekezaji ikiwa ni pamoja na ubia baina ya sekta ya umma na sekta binafsi kwa lengo la kuwajengea uwezo wa namna ya kutekeleza miradi ya ubia.” Waziri wa Maji Bungeni, Mei 2018.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati Waziri anaeleza hii kama changamoto, benki binafsi inanyang’anywa kazi ya mradi muhimu wa kupunguza gharama za uendeshaji wa miradi ya maji vijijini. Sekta binafsi itapata wapi matumaini ya kushiriki kwenye sekta ya maji?

Mheshimiwa Naibu Spika, Benki ya Dunia inapanga majaribio ya kutumia umeme wa jua kuendesha miradi ya maji vijijini kwa kutoa mkopo nafuu kwa Jumuiya ya Watumiaji wa Maji (COWSOs) kwa kushirikiana na taasisi za fedha nchini. Baada ya Benki ya Dunia kukamilisha mchakato wa kupata benki ya kufanya kazi hiyo ya kukopesha COWSOs, Serikali imeilazimisha benki hiyo kutoa kazi kwa benki nyingine ambayo kwa sasa inaelekea kuanguka kutokana na kuwa na mikopo chechefu mingi na changamoto za uendeshaji. Serikali inapotaka sekta binafsi kushiriki kwenye sekta ya maji au sekta yoyote nyingine na wakati huo huo kuweka vikwazo, huu ushuriki wa namna gani?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini Katibu Mkuu Hazina anataka benki iliyoshinda zabuni ya kutekeleza mradi huu muhimu iondolewe badala yake TIB wapewe kazi ambayo walishindwa na kuamua kujitoa na kwamba pia hawana uwezo wa kuifanya? Hii ni pilot tu kwa nini Hazina wasiache ifanyike ili ikiwa na mafanikio ndipo Benki ya Serikali iingie kwa mradi mkubwa? Nina zabuni ya mradi huu wa majaribio, Bunge likihitaji litawasilisha. Bunge liitake Serikali iache kuingilia mchakato huu ili tuweze kuona majaribio haya yana faida gani kwa nchi kabla ya ku-scale upya hii project.