Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Lathifah Hassan Chande

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. LATHIFAH H. CHANDE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi hii ya kuweza kuchangia kwenye Wizara hii ya Maji.

Awali ya yote napenda kuzungumzia kuhusiana na suala zima la kutunza vyanzo vya maji. Tunatambua kwamba mabadiliko ya tabianchi na ongezeko la shughuli za kibinadamu linapelekea hali hatarishi kupelekea kwenda kukosa maji katika siku za usoni. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikitumia mabilioni ya fedha kwenye miradi ya usambazaji wa maji, lakini imeacha kujiwekeza katika suala zima la kutunza vyanzo vyetu vya maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naweza kusema kwamba Serikali imeshiriki katika kuhujumu vyanzo vya maji. Kwa nini nasema hivyo? Ni kwa sababu haijaweka kipaumbele kwenye suala hili hata katika hii bajeti ambayo inaenda kupitishwa hamna fedha zilizotengwa kwa ajili ya kutunza vyanzo vya maji. Miradi hii ambayo ikitumia mabilioni ya fedha sustainability yake itakuwaje, maana yake itakuwa ni miradi isiyo endelevu kama vyanzo vyenyewe vya maji hakuna mkakati wowote wa kuvilinda.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali haijaweka mpango wa muda mfupi wala wa muda mrefu katika suala zima la kutunza vyanzo hivi vya maji. Nasema hivyo nikitambua kabisa nchi nzima hili tatizo limejitokeza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutoa mfano wa Lindi na Kilwa Kusini tangu enzi za wakoloni kuna mto mmoja unaitwa Mto Mavuje ulikuwa una uwezo wa kusambaza maji kwenye kata nne, Kata za Pande, Kilwa Masoko, Limalyao na Kivinje. Enzi za wakoloni walizuia maji kwenye mto ule wakaweka na mageti lakini leo hii mageti yale yameanguka Serikali haijachukua hatua yoyote ya kuweza kwenda kuyarudishia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, siyo hivyo tu, Serikali hii hii ilichokifanya imeingia mkataba na mwekezaji wa nje Bio Shape kwa ajili ya kuja kulima mimea ya nishati. Bio Shape alikuja hapa kwa ajili ya mradi huo, cha kushangaza mradi huo ulihitaji awe anakata misitu, kwa hiyo akakata miti katika eneo hilo la mto na mradi huu umeota mabawa. Ameenda kukata miti kwenye mto huo, kumebaki jangwa na mto huo sasa unashindwa hata kuhudumia kata nne kama ilivyokuwa enzi za wakoloni. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la maji ni la kidunia siyo kitaifa tu, ndiyo maana unakuta nchi za wenzetu Serikali inachukua hatua katika kudhibiti vyanzo vya maji. Mfano naweza nikatoa Australia, wameweka udhibiti kwa kuhakikisha kwamba wale wanaoingia katika maeneo ya vyanzo vya maji wanatozwa, kwa hiyo inakuwa fundisho kwa watu wengine. Siyo huko tu, South Africa wameanzisha kampeni ya Water Wise, ambayo inahamasisha na kuelimisha wananchi juu ya utunzaji wa vyanzo vya maji, kwa nini sisi Tanzania tushindwe? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama Wizara ya Maliasili na Utalii imeweza kushirikiana na TANAPA katika kudhibiti watu kuingia na kufanya shughuli hovyo katika hifadhi za misitu na maeneo ya mbuga za wanyama, kwa nini ishindikane kuja na mfumo/mpango madhubuti kwa ajili ya kuweza kudhibiti na kutunza vyanzo vyetu hivi vya maji huku tukitambua kabisa kwamba Serikali inatumia pesa na mabilioni ya pesa katika miradi mbalimbali ya maji ambayo haiwi endelevu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano mwingine ni Stiglers Gorge ambao hautokuja…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)