Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru kwa kunipa dakika tano kwa sisi wataalam wa habari dakika tano ni muhtasari tu wa habari. Kwa hiyo, nitaenda straight.

Mheshimiwa Naibu Spika, bila kupoteza muda nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu kaka yangu Kitila kwa kazi nzuri mnayofanya. Mwaka jana kwenye Bunge hili nilitoa maombi kwamba iundwe Tume Maalum ya kuchunguza miradi ya maji. Mwaka huu wakati wa Ofisi ya Waziri Mkuu nilitoa ombi hilo hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi mingi ya maji ni zaidi ya makinikia, naomba Bunge liunde Tume huru ya Bunge ichunguze miradi ya maji. Nimemsikia kaka yangu hapa akisema, Mheshimiwa Rais ameanza kuchukua hatua hakuna sababu, tusimwache Rais peke yake, Bunge lina nafasi yake kama muhimili, likachunguze miradi hii ya maji lakini wakati Bunge linaunda Tume hiyo na watu wa Mambo ya Ndani wajiandae kupanua Magereza. Miradi mingi ya maji kwa Wabunge tunaotoka vijijini imekuwa ni deal tu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikupe mfano mmoja mdogo sana, Chemba pale tuna miradi mitatu, kwa mfano Mradi wa Goima aliyepewa ukandarasi alikuwa Afisa wa TAKUKURU. Mimi nimemkuta site huyo Afisa wa TAKUKURU ndiye Mkandarasi aliyepewa mradi wa Maji wa Goima na sasa hivi amekimbia kabisa hata Kondoa hayupo. Kelema Kuu pale umechezewa tu, hela inachezewa tu hivi halafu tukisema humu ndani tunaonekana kama watu wa hovyo hivi, hapana! (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri ninaomba hata ukizunguka kukagua miradi yote Tanzania bila kuchukua hatua na ukaunda tume ya kukusaidia wewe kesho na kesho kutwa utaonekana hujafanya kazi, utapanda kwenye matenki, huwezi kupanda kwenye matenki yote Tanzania nzima. Umri wako nao unakwenda, unafanya kazi nzuri sana, lakini mwisho utakuja kuanguka kwenye matenki bila sababu. Jambo la kwanza ni kuunda Tume huru ya Bunge ifanye uchunguzi nchi nzima, miradi mikubwa na midogo inapigwa. Pili, ninakuomba Mheshimiwa Waziri mmeshafanya tathmini Bwawa la Farkwa wananchi wanasubiri fidia wako tayari kupisha ujenzi wa mradi ule wa maji. Tatu, hizi COWSOs mnazosema ni sera ya Taifa ya maji wananchi hawana utaalamu wowote wa kusimamia miradi ya maji, mkishatumia shilingi milioni 500 mnakabidhi kijiji mradi wa maji baada ya miezi miwili ama mitatu mradi unakufa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sera inaweza ikabadilishwa, badilisheni hii Sera ya COWSOs tuangalie namna gani ya kusimamia miradi hii ambayo imekamilika lakini leo unatengeneza mradi baada ya miezi miwili unakufa, unawakabidhi mradi wanakijiji hawana utaalamu wowote unawaambia mtasimamia huu mradi, badilisheni hii sera. Wamewaletea wazungu ikifika wakati haifai badilisha, wananchi tunachotaka ni maji siyo sera nani asimamie mradi wa maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nne, Mheshimiwa Waziri ninakuomba kwa dhati kabisa njia sahihi ni kujenga mabwawa. Chemba kule tunaomba hela ya mabwawa mawili kati ya Kinkima na Churuku, kati ya Itolo na Mlongia hatuna matatizo yoyote na kujenga Bwawa la Kisangaji kule Kondoa, lakini Kondoa mmetugharimu sana kwenye Mradi wa Maji wa Ntomoko, na leo watu karibu zaidi ya 18 wanahojiwa kule Kondoa, ninampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kuchukua hatua hiyo, tujengeni mabwawa tumalize hilo tatizo.

Pia Mheshimiwa Waziri nikuombe hivi hawa DCCA wameenda kutuibia kule, wamechimba kisima cha maji pale Ovada shule ya sekondari fedha ya Serikali wamelipa milioni 32 hicho kisima hakina hata maji, tumechimba kisima kingine what kind of this? Mpaka DCCA kampuni ya Serikali nayo wezi! Nilikuwa najiuliza hivi wanalipwaje hawa watu hakuna maji? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, ninakuomba pamoja na kuunga mkono hoja…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kw amuda wa Mzungumzaji)