Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukru. Nami niweze kuchangia Wizara hii muhimu sana, Wizara ya Maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, maji ni uhai lakini pia maji ni uchumi. Kwanza kabisa nianze na Jimbo langu la Tarime. Ukiangalia kitabu hiki page namba 175 ningependa kuja kupata ufafanuzi wa kina kwa sababu hizi fedha ambazo mmezi-allocate hapa na kusema miradi imekamilika kwa asilimia 100 ni vitu viwili tofauti. Pia page number 180 maji ambayo tunapata Tarime yanatokana na chanzo cha Bwawa la Nyanduruma. Bwawa hili ni tangu enzi za Mjerumani mpaka sasa hivi halijafanyika ukarabati wowote limetekelezwa, alipokuja Waziri Mkuu alielekeza na Katibu Mkuu ulikuja na timu yako, nashangaa kwenye kitabu bado mmeendelea kutenga shilingi milioni 300 ambazo mmekuwa mkizitenga miaka miwili au mitatu iliyopita bila kuzileta. Ningependa kuweza kupata ufafanuzi wa kina, ile timu iliyokuja iliweza kufanya utafiti upi na imeweza kushauri vipi ili lile bwawa liweze kutengenezwa kwa muda mfupi wakati tukisubiria chanzo kikuu ambacho nimekuwa nikipigia kelele hapa cha maji kutoka Ziwa Victoria ambayo itakuwa ni suluhisho kwa Wilaya ya Rorya, Tarime kwa maana ya Jimbo la Vijijini na Jimbo la Mjini.

Mheshimiwa Naibu Spika, maji ya Ziwa Victoria ni sehemu fupi sana ambayo yanatolewa, Shirati Jimbo la Rorya ambayo inaweza ikaleta Rorya na Tarime lakini imekuwa ni kizungumkuti kwa Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi kuhakikisha kwamba inawaletea wananchi wa Tarime na Rorya maji ili waweze kufanya shughuli zao zingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nirudi kwenye hoja ambazo ni za kitaifa zaidi. Tumeshuhudia kabisa Serikali ya Chama cha Mapinduzi ikiwaambia Watanzania kwamba Sera ya Maji tutapata maji ndani ya mita 400 lakini Awamu hii ya Tano wakaja wakatuambia kwamba wanamtua mama ndoo kichwani.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi ni vitu viwili tofauti, wanaahidi hawatekelezi, wanapanga hawatekelezi na hii inajidhihirisha kwa hizi bajeti ambazo tumeweza kuziainisha. Bajeti ya mwaka 2015/2016 wlileta hapa Bungeni tukawatengea shilingi bilioni 485 lakini wakaweza kupeleka kwenye fedha za maendeleo shilingi bilioni 136 tu, ambayo ni sawasawa na asilimia 28. Ikaja mwaka 2016/2017 shilingi bilioni 913 wakapeleka shilingi bilioni 230 ambazo ni asilimia 25.7 tu. Mwaka 2017/2018 wakarudi tena wakaomba shilingi bilioni 623 lakini mpaka Machi ingawa Waziri ameendelea kusema zimekuja zingine, zilikuwa zimeenda asilimia 22 tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hoja hii utaona kabisa Serikali ya Chama cha Mapinduzi haina dhamira ya dhati ya kutatua tatizo la maji kwa Watanzania. Watanzania ambao, akina mama wanatembea usiku kutafuta maji, wanaliwa na mamba, wanaliwa na fisi, wanapata talaka, wanabakwa, wanapata magonjwa mbalimbali ya vichocho kwa sababu maji ni mabaya, watoto wetu chini ya miaka mitano wanafariki kwa sababu maji si safi na salama, leo Serikali ya Chama cha Mapinduzi inaendelea kuwahadaa Watanzania kwamba wana dhamira ya dhati ya kutatua tatizo la maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ili niweze kuungana na Mheshimiwa Mnyika ambapo jana alipendekeza tumalize michango yetu, leo jioni Wizara isihitimishe bali waende wahakikishe kwamba bajeti tuliyoitenga mwaka jana ambayo inamalizika Juni, iweze kupelekewa fedha walau ifikie asilimia 80 tutatue matatizo ya maji vijijini na mijini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, juzi niliona Katibu Mkuu ametoa takwimu na hapa wamezirudia wakisema kwamba maji kwa vijijini asilimia 59 ingawa najua hii ni average, kuna vijiji havina maji kabisa, hata ukibaki kwenye asilimia 59 yenyewe na World Bank wamesema ni asilimia 50 utaona kabisa kwamba hamna ile dhamira ya dhati. Asilimia 59 hii ndiyo iliyokuwepo kwenye Awamu ya Nne mwishoni, sasa ndani ya miaka miwili na nusu, Serikali ya Chama cha Mapinduzi Awamu ya Tano haijafanya chochote bado ime- stuck kwenye asilimia 59. Huu ni uhalisia kwamba maji siyo kipaumbele, tunatenga billions of money lakini hawapeleki fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jana ndugu yangu Mheshimiwa Anna Gidarya alifanya analysis hapa kwamba kuna kijiji kimojawapo Hanang wananunua maji lita 200 kwa shilingi 7,000. Kwa shilingi 7,000 kwa mwaka unatumia shilingi milioni 2.5, pato la wastani la kila Mtanzania ni shilingi milioni 2.1. Ina maana huyu anatumia pato lake zaidi kwa asilimia 119 kununua maji tu, bado mahitaji mengine na maji ya vijijini siyo safi na salama, hayajawa treated kama maji ya mjini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ili Taifa liendelee, lazima tuboreshe huduma za maji. Maji ni uchumi, bila maji hamna viwanda ambavyo mnasema Serikali ya viwanda. Maji ni uchumi, bila maji hamuwezi kujenga hizo barabara, bila maji hata magari tunayotumia hayawezi kwenda. Kwa hiyo, maji ni kila kitu. Taifa ambalo unataka liendelee lazima tuweze kuwekeza kwenye maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu kingine ni kuhusiana na ufisadi ambao wa kweli umekithiri kwenye miradi ya maji. Tunatenga bajeti zinakwenda kidogo lakini hata hiyo kidogo na yenyewe inafisadiwa na hatuoni hatua zikichukuliwa pamoja na kwamba Serikali ya Awamu ya Tano mnasema mna-fight ufisadi, tunataka tuone kwa vitendo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano tu kwenye ripoti ya CAG anasema kuna mradi ulikuwa Geita ulikuwa ni wa shilingi bilioni 6.6 ambao ulisainiwa Mei, 2015 na ulikuwa ukamilike ndani ya mwaka mmoja, kati ya kampuni ya MSJC and Company Ltd. mpaka Novemba 2017 mradi haujakabidhiwa, fedha zilitolewa zote na zilikuwa za mfadhili (African Development Bank) hatua hazijachukuliwa, kitu cha ajabu wamefanya tu kumtoa Meneja wa Maji Geita, wamempeleka Wizarani. Kumhamisha kutoka eneo moja kumpeleka eneo lingine!

Mheshimiwa Naibu Spika, hii haikubaliki na katika mantiki hiyo tunajua kuna miradi mingi Tanzania nzima imefisadiwa, tunaomba kabisa, siyo Tume, tuunde Kamati Teule ya Bunge ambao ndiyo tunaisimamia Serikali ili tuweze kuhakikisha inapita kwenye miradi yote kuainisha ufisadi umesababishwa na akina nani ili hatua ziweze kuchukuliwa. Vinginevyo tukisema tuunde hii tume kama ambavyo wenzangu walisema awali, inaenda, inajadiliwa juu kwa juu hatujui wahusika ni akina nani, Bunge tunaisimamia Serikali tuweze kuunda Kamati Teule ya Bunge iende ipitie kama ambavyo imeshafanyika huko nyuma kwenye Nishati na Madini enzi za Jairo, tuliunda Kamati Teule ya Bunge ikaja na majibu hapa tukaweza kupata ufumbuzi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye maliasili na utalii tuliunda kuhusu ile operesheni tokomeza ikaja na majibu hapa tukapata ufumbuzi. Miradi ya ufisadi ya maji ambayo tunatumia kodi za wananchi maskini imekithiri ilhali Watanzania wakiendelea kufa kwa kukosa huduma bora ya maji. Tuunde Kamati Teule ya Bunge.

T A A R I F A . . .

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, at a time, we don’t need to waste time!

Mheshimiwa Naibu Spika, hili ni Bunge, linaisimaia Serikali, unavyoniambia Rais katoa kauli wakati nimetoka kusema hapa Mtendaji wa Geita amefanya kuhamishwa kupelekwa Wizarani, tafadhali sana, tusiwe tunapenda kuingiliana kwenye kuchangia kama unajua unatoa hoja ambayo haina mantiki, tuko serious hapa kufanya mambo ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi ambayo inachukua muda mrefu bila kukamilika, ambayo inazidi kuongeza gharama kwa fedha za Watanzania walipa kodi maskini, utakuta miradi inachukua zaidi ya miaka saba haijakamilika na kuhakikisha kwamba shilingi yetu thamani yake inazidi kushuka kila siku ukilinganisha na dola, kwa hiyo gharama za mradi zinazidi kuwa kubwa zaidi na huu unakuwa ni mzigo kwa Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano wa hii ni ule mradi wa Bwawa a Kidunda, Kimbiji na hata Mpera, umechukua miaka mingi sana, kwa nini Serikali inapoteza fedha za Watanzania kwa kuacha kukamilisha hii miradi?

Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie kwa kusisitiza Serikali ya Chama cha Mapinduzi jana Wabunge wenzangu waliongea hapa mkawa mnawadhihaki, Serikali ya Chama cha Mapinduzi msiwekeze kwenye maendeleo ya vitu wekezeni kwenye maendeleo ya watu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa analysis ile ambayo mliisimamia jana mkatoa na miongozo hivi kwa akili ya kawaida kabisa vipaumbele vyetu ni vipi, kununua ndege ambayo only 5% of Tanzanians ndiyo wanatumia na kwa wengine is not even a basic need hiyo ni it’s a luxury need. Ni nini ambacho tunaanza nacho kama nilivyosema awali kwamba maji ni uchumi, unasema kwa sababu ya utalii ulete fedha. Hivi mtalii gani atakuja anaingia hotelini akifungua bomba linatoa maji kama chai ya rangi, wakati alipotoka unatumia tap water kunywa maji straight, tujiulize mara mbili tuboreshe kwanza kuhusu maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo unawekeza kwenye ndege asilimia tano ya Watanzania wanatumia, unaacha asilimia mia moja ambayo ni maji kila Mtanzania anahitaji, viumbe hai vinahitahi hayo maji, mimea inahitaji maji and then mnakuja mnalihadaa Taifa kwamba tumewekeza kwanza kwenye ndege ambazo zinaleta utalii.

Mheshimiwa Naibu Spika, hizo ndege ambazo zinaleta utalii let’s start with things ambazo tukiwawezesha Watanzania wetu hawataugua, watakuwa na afya, watafanya kazi, uchumi utapanda kuliko ilivyo sasa hivi and then automatically tutanunua hizo ndege tutajenga viwanda, tutafanya vitu vingine vyote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie kwenye maji. tumeshuhudia kwamba….

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.