Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii na mimi niweze kuongea machache.

Mheshimiwa mwenyekiti, kwanza kabisa nianze kwa kuipongeza Serikali kwa mipango mizuri kabisa. Tunapojadili kuhusu maji tunajadili maisha ya watu na unapojadili maisha ya watu hakuna utani lazima tuwe serious, tufanye kazi na lazima tutekeleze kile ambacho tunakijadili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii ya Maji ni Wizara muhimu sana katika Wizara zote. Katika Wizara zote wananchi pamoja na Wabunge tunaweka macho kwenye Wizara ya Maji. Maji vijijini na mijini kama hakuna maji hakuna maisha. Tunasema maji ni uhai na tunapoesema maji ni uhai maana yake mwananchi lazima apate maji na tunaposema kumtua mama ndoo kichwani na iwe ni ukweli tunaitua hii ndoo kichwani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali, tukipanga bajeti ya maji na fedha lazima tuwape kama tulivyopanga. Ni vigumu sana Serikali ikiwa inapeleka kwenye Wizara hii fedha kidogo sana halafu miradi haiishi kwa muda unaotakiwa. Kuna wakandarasi wengi wako site mpaka sasa hivi hawajapata pesa, wanashindwa kutekeleza miradi ya maji kwa sababu fedha hawajapata, kwa hiyo, niiombe Serikali tuache mambo mengine yote, lakini tuhakikishe kwamba miradi ya maji inaisha kwa muda unaotakiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo langu la Mufindi Kusini kuna Mradi wa Maji Sawala unakwenda karibu mwaka wa 12, bahati nzuri sana leo Waziri nimeongea naye, Mawaziri wote wawili, Katibu Mkuu nimeongea nae pia, kwa kweli nilikuwa nimepanga tofauti lakini kufuatana na mazungumzo tuliyoongea naishukuru Serikali kwa mazungumzo tuliyofanya leo. Wamenihakikisha kuwa Mwezi Mei huu fedha zitapelekwa kule kwenye Kata ya Mtwango, kuhakikisha Mradi wa Sawala unatekelezwa kama ulivyopangwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni aibu kubwa mradi wa shilingi milioni 800 au mradi wa shilingi bilioni mbili unachukua miaka sita, saba ni aibu! Bahati nzuri sana Waziri tulienda siku ile kwenye Kata ya Mtwango tukasaini mkataba mbele ya wananchi. Wilaya imeleta maombi toka mwezi wa Machi mpaka leo hawajapata fedha na tuliwaahidi wananchi. Kwa vile Waziri leo umeniambia maneno mazuri ndiyo maana naipongeza Serikali kwenye hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine katika Jimbo la Mufindi Kusini kuna tatizo kubwa sana la maji, kuna matenki ya maji kule karibu Kata 11, matenki yapo Serikali ilijenga kwa ushirikiano na wananchi, miaka ya nyuma miaka ya 1980 ni ukarabati wa miundombinu. Mimi Mbunge nimeleta maombi mara nyingi kwamba kule siyo miradi mipya, ni miradi ambayo inatakiwa kufanyiwa ukarabati lakini hatufanyi hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba Serikali kwenye Kata ya Igowelo, wananchi wanapata taabu sana ya maji, matenki yapo na sources za maji zipo, ni ukarabati wa miundombinu, naomba sana Serikali Igowelo pale ipeleke maji. Ukienda pale Nyololo bahati nzuri Waziri unapita kila siku pale, siku nyingine nenda pale shuka omba maji kama watakupa maji pale, maji hayapo, tunatumia maji ya visima tu ndiyo vinatusaidia vingine visima vile vya kienyeji, wakati tuna mabwawa makubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Kata ya Nyololo ipewe maji, Itandula, Idunda, Mbalamaziwa, Nyololo, Luhunga hizi Kata zote maji hayapo ni habati nzuri sana nawashukuru sana wafadhili wamenisaidia sana wamenichimbia visima kule, sasa hivi tusingekuwa na visima vile ambavyo nilichimba mimi kwa kushirikiana na wafadhili wananchi wasingekuwa na maji mpaka leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba sana Serikali kwenye Jimbo la Mufindi Kusini naomba sana maji yapelekwe kwa muda kama tulivyopanga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona kwenye bajeti kuna fedha imetengwa. Sasa hii fedha ambayo tumeipata hata ikiwa ni kidogo basi ikafanye kazi. Tukipanga shilingi bilioni mbili, basi ziende shilingi bilioni mbili siyo upange bajeti ya shilingi bilioni mbili wewe unapeleka shilingi bilioni moja inakuwa bado haisaidii. Wakandarasi wale wamekopa fedha kutoka benki na wanadaiwa na benki lakini Serikali bado haijawalipa fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa sababu Mheshimiwa Waziri ameniahidi kwamba Mwezi Mei Mufindi hela zinakwenda. Ahsante sana.