Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, bado kuna tatizo kubwa la wanafunzi kuwa na uwezo wa kusoma, kuhesabu hata kuandika katika shule zetu za msingi za Serikali. Hii inatokana na ripoti ya dunia ya 2014. Watu wengi wanakosa ujuzi wa mbinu za elimu za kufundishia. Hii inachangia pia na watu wengi kutokupata motisha kazini, hawalipwi madai yao; sehemu kama vijijini unakuta hakuna nyumba za walimu za kuishi, shule nyingine hazina madarasa, baadhi ya wanafunzi huketi chini, hakuna vitabu, baadhi ya shule unakutana na walimu wawili tu na ndio wanafundisha masomo yote kuanzia darasa la awali mpaka darasa la saba. Je, kwa vitendo hivi patakuwepo na ufaulu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, takwimu zinaonesha idadi ya walimu wa shule za msingi imeshuka kutoka walimu 191,772 mwaka 2016 hadi kufika 179,291 mwaka 2017. Hili ni anguko la 6.5% na kupelekea mwalimu mmoja kufundisha kwa uwiano wa 1:50 ukizingatia uwiano unaokubalika ni mwalimu 1:25.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuwa na nyumba imara lazima msingi uwe imara. Hii inapelekea mpaka kuelekea sekondari, wanafunzi hawafanyi vizuri sababu ya upungufu wa walimu wa hisabati 7,291, baiolojia upungufu 5,181, kama upungufu 5,373; na fizikia 6,873. Takwimu hizi zinatokana na BEST 2016.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika karne hii ya sayansi na teknolojia hapa Tanzania Serikali itakuwa inatafuta wataalam kutoka nchi za nje. Sioni ni kwa jinsi gani tunaweza kuzalisha wanasayansi wetu kwa mtindo huu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali ina mikakati gani wa kushughulikia tatizo la upungufu wa walimu wa shule za msingi na sekondari? Kwa mwaka 2018 Serikali imejipanga kuajiri walimu wangapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni muhimu sana kuwekeza katika elimu, lakini bajeti imekuwa ikiidhinishiwa bajeti pungufu, mfano mwaka 2017/2018 Bunge iliidhinisha shilingi bilioni 4.7064 kwa sekta ya elimu, lakini ilipungua kwa 1.3% ikilinganishwa na bajeti ya mwaka 2016/2017 ambayo ilikuwa ni shilingi bilioni 4.7707 nayo ilipungua kwa shilingi bilioni 64.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado Serikali inashindwa kutenga 20% ya bajeti kwa ajili ya sekta ya elimu na kupelekea Wizara kushindwa kutimiza majukumu yake. Kwa mwelekeo huu, ubora wa elimu hapa nchini hauwezi kupanda hata kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo ni jukumu la Serikali kuhakikisha inatenga fedha za kutosha ili waweze kutenga fedha za kumsaidia mtoto wa kike aweze kuhudhuria shuleni kwa siku zote, kuhakikisha vyoo vyote vinakuwepo na maji na kuwekeza katika utoaji wa taulo za kike bure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini walimu watalipwa posho na madai yao yote ukizingatia wengine wapo katika mazingira magumu sana ya kazi, wengine wana mikopo na kadhalika?