Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ENG. RAMO M. MAKANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Naibu Makatibu Wakuu, wataalam na wasaidizi. Hongereni sana kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni skills development levy; kwa kuwa Wizara ya Elimu ndiyo yenye dhamana, ni vyema ikashauri vyema zaidi juu ya madhumuni ya msingi ya uanzishwaji wa tozo hii. Ni skills zipi zilikusudiwa? Je, kuna mabadiliko ya aina ya skills? Je, ukusanyaji wa tozo hii wa matumizi yake unahitaji kufanyiwa marejesho? Kwa kifupi, jambo hili linatakiwa kutazamwa upya kwa makini zaidi na kwa kushirikisha wadau (wachangiaji) ili na wao wapate huduma zaidi ya kuendelea kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kuhusu Vyuo vya Ufundi Stadi. Wilaya ya Tunduru jiografia yake ikiweka mbali sana na Vyuo va Ufundi. Hivyo kuwafanya wahitimu wa elimu ya msingi na hata wa sekondari kukosa fursa hiyo ambayo ingeweza kuwakwamisha kiuchumi na wakachangia uchumi wa Taifa. Pia tunamwomba kuwa considered.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, inawezekana kupandisha hadhi Chuo cha Maendeleo ya Jamii Nandembo na kuwa Chuo cha VETA na elimu zote zikatolewa hapo hapo? Tunaomba kuwa miongoni mwa wanufaika katika miradi ya ujenzi wa madarasa na matundu ya vyoo kama ilivyoidhinishwa katika kitabu cha bajeti ukurasa wa 124 (item iv).