Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Muhammed Amour Muhammed

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Bumbwini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote ni vema nikamshukuru Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na ardhi, mwingi wa rehema. Pia nakupongeza wewe binafsi kwa jinsi ulivyokuwa makini katika kulisimamia Bunge letu na kwa umakini mkubwa sana. Ninaomba kuchangia katika maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kuhusu ufaulu mbaya na usiofurahisha kwa wanafunzi wa kidato cha nne na cha sita. Kwa kweli asilimia ndogo ya ufaulu wa chini ya asilimia 30 siyo mzuri, ni vyema Wizara ingepanga haraka utaratibu mwingine kuhusiana kuongeza taaluma kwa walimu (in service training) kwa mada ambazo baada ya utafiti zingebainika kama zina matatizo kwa walimu wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni National Examination Supervision, kumekuwa na kero zilizoambatana na masikitiko ya kwamba ni walimu gani wenye sifa za kusimamia hii mitihani? Kuna wakati walimu wa chekechea pia hawapewi fursa kusimamia mitihani ambapo ni kinyume na utaratibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kuhusu nyongeza ya mishahara ya walimu. Idadi ya wanafunzi inaendelea kuongezeka na walimu wamekuwa wakiendelea kufundisha katika mazingira magumu sana na kipato chao kinaendelea kushuka na kuonekana walimu nchini ni watu dhaifu sana na maskini. Ni vyema bajeti ya elimu iwe ni pamoja na kuwaongezea mishahara walimu. Hili liangaliwe sana ili kuwalinda walimu wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.