Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza sana Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kunisaidia ujenzi wa mabweni mawili ya shule ya sekondari Malampaka. Haya ni nyongeza ya mabweni mengine yaliyojengwa baada ya Waziri wa Elimu kutoa fedha pia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa wakati wa kuwa na refa wa ubora wa elimu wa kitaifa ambaye atakukwa huru kufuatilia ubora, usimamizi na uendeshaji wa shule zetu za msingi na sekondari. Huyu atasimama katikati ya shule binafsi na shule za Serikali. Refa huyu atafanya the playing ground kuwa leveled kati ya shule ya Serikali na shule binafsi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wakati muafaka sana Serikali ije na mapendekezo ya kuunda chombo hiki ili kisaidie kuendesha shule zetu za msingi na sekondari kwa usawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni upungufu wa walimu na vitabu katika Wilaya yangu ya Maswa hususani Jimbo langu la Maswa Magharibi. Katika shule za msingi tuna upungufu wa walimu 727. Shule za sekondari tuna upungufu wa walimu 108 wa masomo ya sayansi na walimu 88 wa masomo ya sanaa hasa kiingereza. Naiomba Serikali wakati wa kugawa walimu wanapoajiriwa iangalie maeneo yaliyo na upungufu mkubwa ili yapewe kipaumbele kama ilivyo Wilaya yangu ya Maswa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia tuna upungufu wa vitabu vya masomo ya sanaa upande wa sekondari. Vitabu vya darasa la nne kwa mtaala mpya havipo kabisa mkoa mzima wa Simiyu. Naiomba Serikali itatue changamoto hii ili watoto wetu wapate elimu bora si bora elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vyuo vyetu vya maendeleo ya jamii bado vinaweza kutoa ujuzi na utalaamu tunaouhitaji ili kuendeleza masuala ya ufundi kwa watoto wetu. Hata hivyo vyuo hivi vina miundombinu iliyochakaa sana. Moja ya vyuo hivyo ni Chuo changu cha Maendeleo ya Wananchi cha Malampaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana Wizara iangalie ni kwa namna gani chuo hiki kinaweza kukarabatiwa na kupatiwa vifaa vya kufundishia pamoja na kuongezewa walimu. Vilevile naomba Serikali iangalie upya mitaala ya kufundishia ya vyuo hivi. Kwa maoni yangu mitaala iliyopo ni ya zamani haiendani na mazingira tuliyo nayo sasa hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana naomba kuunga mkono hoja.