Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni kwa namna gani mfumo wetu wa elimu unaomuandaa kila mwanafunzi kwenda chuo kikuu, unawaandaa vijana kuingia katika mfumo wa Tanzania ya viwanda kama tunavyojadili Tanzania ya viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, mhitimu wa chuo kikuu wa Tanzania ni mwanafunzi wa aina gani? Mtu aliyefuzu katika sera ya policy maker ndiyo huyu anaenda kwenye utaalamu wa kuendesha na kusimamia viwanda (uchumi wa viwanda). Nashauri mfumo wa elimu yetu ubadilike kabisa, kuwepo na mjadala wa kitaifa, watu waseme tunahitaji wahitimu wa namna gani. Mfano, tunaweza kuwa na mfumo wa darasa la kwanza mpaka la nane, then miaka miwili au mitatu ya kum-train mtu katika ujuzi fulani (specific areas of interest).

Mheshimiwa Mwenyekiti, mjadala wa kitaifa juu ya hatma ya watoto wanaopata ujauzito na ikabainika hawakujitakia (victims) wapewe nafasi ya kurejea shuleni badala ya kinachoendelea sasa hivi. Tafiti zinaonesha kuwarejesha watoto hawa shuleni (waliozaa) hakujaongezea idadi ya wanaopata mimba shuleni, hili suala badala ya kufanya siasa jamii ipime na kuamua kwa kutumia case studies za nchi nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuharakishwa kwa vitabu vya kiada katika ngazi zote ili kutengeneza uelewa wa pamoja, mada za vitabu hivi pia zi-reflect mazingira na mahitaji ya Taifa na utandawazi kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, masharti ya usajili wa shule uzingatie huduma muhimu za wanafunzi ukiwemo uwepo wa miundombinu ya maji, vyoo vya uwiano sawa kwa wanafunzi na madarasa, kuliko tunachokiona leo. Asilimia 60 – 70 ya shule hasa za Serikali hukosa miundombinu, hivyo kuwa kero kwa wanafunzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uanzishwaji wa chuo cha ualimu na vyuo vya ufundi katika Wilaya mpya ya Kyerwa, eneo hili lina vijana wengi lakini hakuna chuo chochote wala high school ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kubagua wanafunzi wa kupewa mikopo kwa kigezo kuwa ametokea shule nzuri sekondari, wanafunzi hawa hawatendewi haki. Pengine walibahatika kupata mfadhili katika hatua hizo. Kwa kuwa huu ni mkopo hawatendewi haki kunyimwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, madeni ya walimu na wahadhiri. CAG ameainisha kuwa Chuo Kikuu cha Ardhi kinadai malimbikizo ya mishahara ya walimu na marupurupu yao, hii inapunguza morali kwa watumishi hao, Wizara iombe Serikali kulipa madeni hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu sera ya elimu bure. Sera ya Elimu Bure haitekelezeki kwa kuwa changamoto ni kubwa sana katika maeneo ya shule hizi, madai ya wasichangie ni mufilisi, pengine kauli mbiu ingebadilika na kuwa changia elimu bure iwe bora, wazazi wangeshiriki kwa chochote kuboresha mazingira ya kufundishia (miundombinu) vyoo, madarasa, vyakula na kadhalika.