Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza sana Serikali kwanza kwa kubuni mradi huu wa shilingi milioni hamsini kwa kila kijiji lakini pia kwa kutambua kuwa pesa hizi pekee hazitoshi na kuongeza fedha za ushauri na usimamizi. Hili jambo jema sana. Kila Wilaya kuwe na desk la consultancy na kuwe na wataalam wa kilimo, biashara, utafiti na kadhalika. Nashauri fedha nyingi katika hii shilingi milioni hamsini ikopeshwe vikundi vya kilimo. Washauriwe vizuri, walime vizuri, kitaalam na baadaye vikundi hivi visindike mazao hayo na kutafutiwa masoko. Tanzania ya viwanda itakuwa rahisi sana kama mapinduzi ya kilimo yatatangulia kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba sana Wizara ilete mageuzi sana kwenye masoko ya wakulima. Wakulima katika maeneo mengi wanauza mazao kwa walanguzi kwa bei ya chini sana. Vyama vya Ushirika viimarishwe, masoko ya uhakika yatafutwe. Utaratibu wa stakabadhi ghalani uenee maeneo yote Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Lupa, Maafisa Ushirika wa Wilaya na Mkoa wanakwamisha juhudi za wananchi kuanzisha Vyama vya Ushirika. Nina mfano wa Vijiji vya Lola na Lyesero, hawa wanakataliwa kuanzisha AMCOS kwa sababu ambazo hazina mashiko.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Wizara itafute wanunuzi wa tumbaku wengine toka China waliopo wameanza maringo na ukiritimba.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.