Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Anna Joram Gidarya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ANNA J. GIDARYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia katika Wizara hii ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni kuhusu uhaba wa walimu. Walimu ni nyenzo muhimu katika nchi yetu lakini kwa muda mrefu kumekuwa na uhaba wa walimu. Pamoja na kuwa vyuo vingi vimetoa idadi kubwa ya walimu waliokidhi vigezo vya kuajiriwa, lakini Serikali imeshindwa kuwaajiri walimu hawa. Katika shule za sekondari zote nchini kuna uhaba mkubwa wa walimu wa masomo ya sayansi. Nashauri Serikali ifanye mkakati wa haraka na wa makusudi kuondoa tatizo hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili ni walimu wa sekondari kupelekwa kufundisha shule za msingi. Tunatambua kuwa tuna uhaba wa walimu katika shule zetu. Kitendo cha Serikali kuwachukua walimu hawa wa sekondari kwenda kufundisha katika shule za msingi si sawa kabisa kwa kuwa kila ngazi ya ualimu ina miongozo ya namna ya ufundishaji kwa masomo husika na madarasa yanayofundishwa na walimu wenyewe. Ni vema sasa Serikali ianze upya utaratibu wa kuajiri walimu kulingana na madaraja yanayotakiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu ni ujenzi wa miundombinu ya madarasa kwa watoto wenye ulemavu. Katika maeneo mengi nchini miundombinu ya madarasa haikuzingatia mahitaji ya watoto wenye ulemavu, jambo ambalo linawafanya watoto hawa kusoma katika mazingira magumu mfano miundombinu ya madarasa, vyoo na hata njia za kupita siyo rafiki kabisa. Nashauri Serikali ihakikishe kuanzia sasa shule zote zinazotarajiwa kujengwa ziwe na mfumo maalum kwa watoto wenye ulemavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nne ni kuhusu Vyuo vya Ufundi (VETA); kwa kuwa kwa sasa kwa kipindi kirefu Serikali haina mpango wa kuajiri pamoja na changamoto nyingi za watoto wengi kutofaulu wanapomaliza elimu ya msingi na hata kidato cha nne na kushindwa kuendelea na masomo jambo ambalo limesababisha wimbi kubwa la vijana mtaani na kuzurura hovyo. Serikali imepoteza nguvu kazi ya Taifa kwa kushindwa kujenga vyuo vingi vya ufundi. Nashauri Serikali ijenge vyuo vingi vya mafunzo ya ufundi kwa kila mkoa kadri iwezekanavyo ili kunusuru kundi hili la vijana wa Kitanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.