Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala langu linahusu kusaidia kufungua Chuo cha VETA katika Wilaya ya Nkasi, Paramawe kwenye majengo ambayo yako kumi na nne tuliyopewa na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Majengo hayo yamekwishakaguliwa na VETA Kanda ya Nyanda za Juu Mbeya na kuridhika kabisa kwani yana umeme na maji. Pia tumetoa eneo la ekari 50 kwa ajili ya Chuo cha VETA Paramawe – Nkasi, kwa hiyo, pa kuanzia tunapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati mbaya sana ziara ya Rukwa, Nkasi Waziri aliahirisha, ilikuwa ufike sehemu yaliyopo majengo hayo mazuri sana. Tunaomba sana msaada wa Waziri. VETA Kanda ilikwishayakubali na kuridhika kabisa. Tunaomba sana msaada wa hali na mali. Majengo yakikaa sana yanaharibika na utunzaji wake ni gharama sana.