Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchukua nafasi hii kukushukuru wewe kwa kunipatia nafasi hii ya kutoa machango wangu katika hotuba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia. Pia napenda kumpongeza kwa dhati Waziri wa Wizara hii pamoja na watendaji wake wote kwa kuandika vyema hotuba yao na kuiwasilisha kwa ufasaha katika Bunge lako tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuchangia hotuba hii napenda kuchangia katika maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni Chuo Kikuu cha Dodoma. Chuo hiki ni miongoni mwa vyuo muhimu sana katika nchi yetu hasa ukizingatia kuwa kiko katika mji mkuu wa nchi yetu. Kinahitaji maboresho ya hali ya juu katika rasilimali watu ili kiende na wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimefurahi kuona kuwa katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri ameeleza kuwa amegharamia masomo kwa walimu/wafanyakazi 377 katika nyanja tofauti. Suala langu katika wafanyakazi hao ni kwamba Waziri hajaeleza wafanyakazi 377 aliowapatia mafunzo ni kati ya wangapi yaani ni asilimia ngapi ya 377 waliopata mafunzo hayo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili ni kuhusu Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi. Naipongeza Wizara ya Elimu kwa kuimarisha mamlaka hii. Hii ni mamlaka inayowagusa wanafunzi wa kipato cha chini na makundi tofauti. Ameeleza namna inavyojitahidi kuongeza vyuo katika maeneo kadhaa nchini. Nashauri katika ujenzi wa vyuo hivyo uzingatie uwepo wa makundi yote. Majengo yawe na facilities kwa ajili ya watu wenye ulemavu ili nao wafaidi matunda ya nchi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.