Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuipongeza Wizara kwa kazi nzuri iliyofanyika chini ya uongozi wake Mheshimiwa Waziri Profesa Joyce Ndalichako (Mbunge) akisaidiwa na Naibu wake Mheshimiwa Dkt. William Ole Nasha (Mbunge). Pia niwapongeze watendaji wote chini ya uongozi wake Dkt. Akwilapo na Naibu wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, binafsi kwa niaba ya wananchi wa Jimbo langu la Nyasa, natoa shukrani nyingi kwa jinsi ambavyo wamelisaidia na leo nimeona tena Chuo cha VETA Nyasa kikiwa katika mpango wa kujengwa, nawashukuru sana. Naomba pia niwatajie wazee wa P4R, DPP wetu Ndugu Gerald na timu yake, kazi haikuwa nyepesi, nasema hongereni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru pia TEA kwa kuliona jimbo langu. Nawashukuru wote kwa upendo toka nikiwa nao hata nilipoondoka. Hali ya jimbo langu ilikuwa mbaya sana kimiundombinu ya elimu. Hata hivyo, nazidi kuomba juu ya Shule ya Lumalo na Shule ya Sekondari Nyasa kuhusu bweni ambalo halijaisha toka SEDP.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nazidi kusisitiza juu ya umuhimu wa kuwezesha R&D Institutions ili kufanya tafiti mbalimbali zitakazowezesha uwekezaji wa tija. Kwa kuwa TIRDO ndiyo jicho la viwanda, kama ilivyo jina lake, niiombe Wizara kupitia COSTECH kuisaidia taasisi hiyo iweze kutimizia majukumu yake na hasa la kufanya mapping ya rasilimali ili hata anapokuja mwekezaji yeyote tuwe tuna taarifa za kutosha. Watafanya kwa kushirikiana na taasisi zetu za vyuo kulingana na aina ya utafiti.