Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa. Awali ya yote nichukue fursa kuipongeza sana Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Daktari John Pombe Joseph Magufuli, lakini pia na timu yake yote ambayo anakwenda nayo. Naona tunakwenda vizuri sana kwenye mwelekeo tunaoutarajia. Pia nimpongeze dada yangu Profesa Ndalichako kwa kazi nzuri ambayo mnakwenda nayo na hotuba nzuri ambayo mmewasilisha hapa, wewe pamoja na Naibu wako Ole Nasha na timu nzima ya Wizara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hotuba nzuri lakini yapo mambo ambayo nadhani kuna kila sababu ya kuyajazia nyama au kuyaboresha hivi. Nitakuwa na mambo machache nikianza na suala zima la walimu.

Mimi nadhani katika kuinua ubora wa elimu katika kuhangaika sana na suala zima la ufaulu wapo wadau kadhaa muhimu sana, wanafunzi, wazazi pia na walimu. Kwenye upande wa walimu, upatikanaji wao na uendelezaji wao nadhani tuangalie vizuri kidogo. Ningependekeza badala ya kuchukua walimu ambao wanakuwa wamefaulu labda daraja la pili au la tatu, ili mtu uwe mwalimu utoke kama top class student ili ukaweze kuwasaidia hawa ambao unajaribu kwenda kuwaelimisha. Kuchukua hawa ambao huku nyuma huku wamefaulu labda wastani na nini inaweza isiwe sawa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua huenda kuna changamoto ambayo tutakumbana nayo hapo mbele lakini napenda sana kusisitiza sana walimu watokane na wanafunzi wanaofaulu juu kabisa kwenye darasa lao. Kama ambavyo kwenye vyuo vikuu wapo wale top student ambao ndio wanaenda kuwa tutorial assistants matokeo yake baadae wanakuwa lecturers huko mbele. Kwa nini nasema hivi tunataka kuboresha elimu tunataka kupata kizazi ambacho kina upeo mkubwa ni lazima upate wenzao wanaowafundisha wawe na upeo mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na ikifikia hapo; najua kuna changamoto mojawapo ya labda kuboresha maslahi ya walimu ambayo ni lazima tuanze mahali. Suala la kuboresha mazingira ya kazi za walimu lazima tuanze mahali. Ifike wakati mtu akisema mimi nakwenda kusomea ualimu anajivuna. Kazi na taaluma ya ualimu iwe ni wito wa kujivunia kama ambavyo tunaona wenzetu wanasheria akikaa anaweka kifua mbele anasema mimi I am a learned brother au architect au madaktari, twende namna hiyo. Huko nyuma kazi ya ualimu ilikuwa na heshima sasa hivi mtu anakwenda ili mradi akafanye kazi. Nasisitiza sana wanaokwenda kusomea ualimu tuwe tunawatoa kutoka wale waliofaulu vizuri kabisa, top class student.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapo hapo ukishawapata hawa walimu umuhimu wa kuwajengea uwezo endelevu unatakiwa. Si ilimradi nimefaulu nimekuwa mwalimu basi naendelea, na muda unapita education yangu huku kichwani inakuwa wakati mwingine obsolete au una-rust, unaota kama kutu hivi. Kuwe na utaratibu wa kuhakikisha hawa watu kuna mfumo na mpango endelevu wa kuwaendeleza, continuous learning, continuous training hapa na pale katika suala zima la kuwapatia capacity building, hilo ni jambo la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili nataka niongelee suala zima la shule zisizo za Serikali. Hizi shule zimeonekana zikifanya vizuri sana miaka yote, tangu huko nyuma. Sasa mimi swali langu najiuliza hapa katika kutafakari, kama hawa wenzetu wanafanya vizuri ina maana wana kitu tunaita best practice, kwa nini tusiwatumie wao, tushirikiane nao ili na sisi tuweze kuboresha huu upande wa kwetu? Yaani ni lazima kuna button nzuri wanazozi-press, the right button zinazowapelekea wafaulu. Suala zima la nidhamu, suala zima la kuwa-strict kwenye uendeshaji wao, mahusiano kati ya mwalimu, mwanafunzi na mzazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini inavyoonekana sasa hivi shule za binafsi, zisizo za Serikali ni kama maadui hivi kwa shule za Serikali, jambo ambalo si sawa. Tuwatumie tuwaweke karibu, tuanzishe utaratibu wa kuwashirikisha kwenye kutengeneza sheria zetu kwenye kutengeneza kanuni, miundo, mifumo, haya matamko yanayotoka haya, maelekezo yanayotoka, miongozo inayotoka basi isiwe kana kwamba inakwenda kuwakandamiza, iwe kana kwamba ina-support their existence kwa sababu ndio wanatunyanyua. Ni lazima tushirikiane nao ikiwezekana na kama itaonekana inafaa kiwepo chombo huru ambacho kitaunganisha pande zote ambazo zitakuwa zinatengeneza mwelekeo mzuri wa elimu yetu. Nasisitiza sana hilo la pili kwamba shule zisizo za Serikali ziwe part and parcel ya kuandaa mikakati yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu ninataka kuongelea suala la vyuo vya ufundi. Najua tumewekeza sana kwenye upande wa elimu ile tertiary, lakini upande wa elimu ya ufundi nako kidogo inabidi tuongeze uwekezaji. Tuweke mkazo kwenye vyuo hivi kwa sababu kwanza inaendana na dhana kubwa tunayokwenda nayo sasa hivi ya uchumi wa viwanda.

Pili, kuna kundi ambalo huwa halifanikiwi kwenda kwenye elimu ile rasmi ya form five na six na hatimaye chuo kingine basi wapite huku kwenda kutengeneza ajira, kuwa- capture wale vijana ambao wanakuwa hawakupata fursa wasije wakazagaa mtaani…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)