Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia fursa hii muhimu na mimi niweze kuchangia kwenye hoja hii muhimu sana ya elimu hasa kipindi ambapo kumekuwa na changamoto nyingi sana. Nishukuru sana kwamba Wabunge wote nadhani tunakubaliana kwamba suala la elimu sasa hivi ni janga la Taifa kwa sababu tunashuhudia mambo mengi yanayotokea na kubwa niseme kwamba katika elimu siku zote nimesema mwalimu ndio kipaumbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo kwa masikitiko makubwa sana Serikali bado haijaliona hilo. Leo walimu wana matatizo lukuki, yamesemwa na wengi. Kuna suala la kupandishwa madaraja, haiwezekani mwalimu alitakiwa apandishwe daraja toka mwaka 2003 mpaka leo yuko pale pale ameenda kusoma bado hajapandishwa daraja na hawa ni wengi na ndiyo sababu takwimu zinaonesha kwamba takribani asilimia 70 hawana morale wa kufundishia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kubwa zaidi mishahara yao bado lakini niseme tu kwamba lingine kubwa katika elimu ni vitabu na mitaala. Huwezi kuwa na vitabu mizuri kama huna mitaala mizuri. Mwaka jana kipindi kama hiki niliongea na watu na wengine walichangia kuhusiana na ubovu wa vitabu katika nchi hii, jambo ambalo linafanya watoto wetu washindwe kusoma vizuri. Kwa sababu tayari walimu hawana morale, kwa hiyo the only alternative tungekuwa na vitabu vizuri wanafunzi hawa wangeweza kufanya vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kitabu kinachoitwa kitabu cha uraia na maadili bendera ya Tanzania, kitabu cha darasa la tatu, ile rangi ya manjano zinaonekana mbili kule wameweka nyeusi yaani leo bendera ya Tanzania mtoto mdogo ambaye ubongo wake ni tete na kila anachoambiwa kina stick bendera ya Tanzania imebadilishwa, nembo ya Tanzania haina zile alama za shoka hazipo. Bendera iliyopo na nitaomba mtuambie hii ni bendera ya nchi gani. Bendera yenye rangi za kijani mbili chini na juu hamna rangi ya blue na katikati rangi nyeusi na hizo njano naomba mtuambie hii ni bendera ya nchi gani? Ukija kutujibu utuambie Mheshimiwa Waziri na Naibu wako, mmewahi kukaa mkapitia hivi vitabu baada ya kuambiwa bilioni zaidi ya mia moja zilitumika mwaka jana na baada ya kuongea sana na aliyekuwa kamishina akaondolewa kazini; ninaomba kujua mmefanya mambo gani au utaratibu gani kama Waziri ni kweli umeona hivi vitabu wewe mwenyewe kama profesa umeviona hivi vitabu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitabu cha kuandika darasa la kwanza mtoto ambaye katika elimu yake ya awali hajasoma kitabu hakuna kitabu chochote cha shule ya awali, hakuna, anaenda kuanza darasa la kwanza kuandika kitabu cha page 117 lakini mbaya zaidi anaingia la pili kitabu cha page 40; what a contradiction? Yaani wa darasa la kwanza ambaye ndio anaanza page mia moja na zaidi, wa darasa la pili page 40. Darasa la kwanza kuandika anaenda siku ya kwanza kuandika anaandika hii; hii anaandika kitu gani? Hili ni somo la kuandika au ni sanaa?

Mheshikmiwa Mwenyekiti, haya mambo haya ndio sababu tunasema hatuwezi kukuabaliana na hili jambo, Nataka Waziri aniambie, tulikuwa na kitu kinaitwa Educational Material Committee (EMAC) ambao hawa ndio ambao walikuwa wanahariri vitabu na committee ikavunjwa kutokana na mambo fulani, mimi naomba kujua baada ya Kamati hii kuvunjwa ni nani wame-replace na ni nani wanahariri hivi vitabu katika hali hii?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo sababu ninasema, na watu wamesema; na ninaomba Wabunge wote waende wasome andiko la Profesa Kasmili Lubagumya waone ni jinsi gani elimu yetu ni mbovu kuanzia huku chini na mimi sishangai university level wakishindwa kuandika barua, aidha ya kiswahili au ya kiingereza kwa sababu huku chini hawakufanya chochote. Huwezi ukaamini wanafunzi wa UDOM anaulizwa jina la Makamu wa Rais hajui. Sasa unajiuliza kama mwanafunzi hajui Makamu wa Rais wa nchi hii, mtoto wa darasa la kwanza la pili hatajua sisi tulivyosoma ilikuwa tunajua yaani kila kitu kilikuwa hapa. Sasa katika hali hii ninaamini Waziri mmeamua sasa kuchukua kwamba nchi hii tunaendeshwa na machivelian principle kwamba inaendelea kuzungumza kuhusu elimu bure. Naomba tusijitoe ufahamu, maana ya bure ni nini? Wakaanza ni bure tulivyopiga kelele wakasema bila malipo, lakini ukisoma kamusi bure maana yake ni kitu kinachotolewa bila malipo yoyote. Ukisoma hotuba ya Waziri Mkuu inasema hivi; “wataendelea kuchangia kwa hiari maendeleo ya elimu kupitia ofisi ya Wakurugenzi” na kwa wale watu wenye miaka yangu na nyuma tunajua Mheshimiwa Chenge ulisoma enzi hizo kwamba tulivyokuwa elimu bure ilikuwa hata kalamu hununui, daftari hununui ilikuwa sana sana ni uniform.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa leo mnapotuambia ni bure wakati michango inaendele haiwezekani na niseme tu kwamba ndiyo sababu shule za private zinafanya vizuri; na Mheshimiwa Waziri nilkuambia na ni rafiki yangu. Kinachofanyika wana kitu kinaitwa Teachers Parent Association yaani huwa utatu huo ndio unaosaidia mnakutana wazazi, walimu na wanafunzi, kama mwanafunzi ana tatizo linaelezwa lakini kwenye shule za Serikali sana ni le bodi ambayo inasubiria shilingi 500 jinsi gani inaenda kugawanywa shuleni, ni vurugu tupu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nilikuwa nadhani hili suala la elimu bure bado halijakaa vizuri na limeleta mkanganyiko mkubwa hivyo inaweza kwa kweli kurudisha maendeleo ya elimu nyuma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie pia suala kubwa hili la mjadala. Sasa niseme, katika hizo changamoto zote nionaomba sasa, kwa heshima kabisa kwamba tumesema report zangu zote au speech zangu zote tumekuwa tukiongelea suala la anguko la elimu na sasa mnaliona. Mnamshukuru mzee Mkapa, pamoja na maneno yote aliyokuwa amesema dhidi yetu kwamba sisi malofa lakini leo ameona kwamba elimu yetu iko vibaya na kwamba tunaenda sasa kufanya kazi; na naomba muongoze huo mjadala ili tuhakikishe kwamba elimu yetu inaboreshwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mwisho nililotaka nilizungumze ni suala la TETRA. Sisi tumeongea kwenye hotuba zetu hiki chombo huru cha kusimamia elimu, haiwezekani, tumezungumza mara nyingi tukasema lazima tuwe…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa, unga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siungi mkono hoja.