Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kipekee kabisa namshukuru Mungu kwa kuwepo sisi hapa salama na tuko katika mambo haya ya maendeleo. Nawashukuru wale wanawake wa Kilimanjaro walioniwezesha kufika hapa na leo nazungumzia jambo la elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu haina mwisho naamini hata Wabunge walioko hapa bado wanajisomesha, bado wanajiendeleza, nichukue nafasi hii kumpongeza sana Profesa Ndalichako na wote ambao wameshiriki katika kuandaa hotuba hii ya bajeti. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende moja kwa moja katika ule ukurasa wetu wa 62 mpaka ukurasa wa 64 wanapozungumzia EP4R. Nimeona wanafanya maandiko tofauti wanapata hela za kutosha wanakarabati majengo, wafadhili wanaenzi shughuli zao. Ombi langu na naomba hata ninyi Wabunge ikiwapendeza iletwe hapa tuazimie hela hizo zisimamiwe na Wizara hii ya Elimu zisiende tena kule TAMISEMI, kwa sababu kama zinapatika na zimekuja na sasa zinafanya jambo la elimu na wengi mmekwenda kutembea mmeona ukarabati hata wa zile shule za zamani kwa nini sasa zinakwenda TAMISEMI, hapo bado inanikanganya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kutoa ombi hilo na pongezi hizo kwa Mheshimiwa ninampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kutoa elimu bila malipo kuanzia darasa la awali mpaka kufikia form four hili ni jambo jema na wazazi wengi wamependa, sasa hakuna sababu ya mtoto yoyote asiende shule. Baada ya elimu hiyo nini kinachoendelea, mwanafunzi akishafunguliwa mlango wa kusoma nawaomba na nawapongeza wanafunzi wote walio mashuleni leo na hata siku za baadae nawapongeza sana kwa kupiga vita ujinga, nawapongeza sana na nawaambia elimu yenyewe ni vita.

Niwaombe tu sasa ukishamaliza form four usibweteke kwamba wewe ni graduate ukae tu, endelea kujiendeleza. Nasema hivyo kwa sababu hata yule graduate aliyemaliza Chuo Kikuu ajira zimekuwa ni shida, kila siku Wabunge wanapigiwa simu wanaombwa wawatafutie kazi, kazi hazipo! Tatizo tu siyo kazi kutokuwepo nadhani hata Walimu na wazazi tunakosea mahali pa kumjenga mwanafunzi au mtoto achukue taaluma gani ambayo mbeleni itamfungua zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa ndani tunasema sayansi, je wewe mzazi unamsisitizia mtoto wako hata kujifunza kuhesabu, kwa sababu msingi wa sayansi ni hesabu. Nawaomba wazazi wote sasa wawe wanapitia vitabu vya wanafunzi wao au watoto wao wajue kwamba wanafunzi hawa wanasoma wanavyotakiwa. Huko mbele tunaona wazi kuna ajira ambazo hazitahitaji tena wafanyakazi, kuna ajira ambazo zinajifuta kwa sababu sayansi sasa imeshafunguka. Kuna fani ambazo sasa hivi zinafanywa na roboti, zinafanywa na mashine, mtu mmoja anakaa anaendesha kiwanda kikubwa, hatuhitaji tena wale mashine operator wengi ni kwa nini sasa wazazi, walimu, wasimwambie mtoto achana kiasi na haya masomo ya sanaa nenda kwenye masomo ya sayansi ambako baadae unaweza kuwa na ajira unayotaka wewe kuingia kwenye payroll.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona kabisa kwamba tulianza kujenga maabara lakini imefika mahali inasuasua, naomba ule mpango wa kujenga maabara uendelezwe. Pia kuwa na maabara bila walimu wa kufundisha sayansi haisaidii, kuna wakati ambapo wazazi tulikuwa tunachangia wale walimu wa sayansi kwa kipindi, ikafika mahali likatoka Toleo la 16 la mwaka 2015 michango isifanyike tena, sasa wale walimu temporary wa kufundisha sayansi mashuleni hawapo tena, nataka ufafanuzi kutoka Serikalini endapo wale walimu hawatakuwepo wale wanafunzi waliopo shuleni sasa hivi watafundishwa na nani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unaona kabisa kwenye maabara tunazungumza kupata walimu wa sayansi, naomba pamoja na walimu wa sayansi tuna wale lab. technician ambao wanafanya maandalizi ya vifaa vya experiment. Naomba wafikiriwe ajira zao ziongezwe tunahitaji lab. technicians ambao wana uzoefu au hata kama ni wageni, lakini wawepo kila lab inalojengwa lipate lab. technicians wawili, kama ni la sayansi labda la physics, chemistry au biology tupate angalau wawili kwa shule moja. Haielezeki tuwe na labs lakini hazina technicians unamtarajia mwalimu huyo aandae vifaa vya experiment mwalimu huyo aje sasa awafanyie vijana hao experiment. Kwa hiyo, hii ajira ya lab. technians naomba sana ifunguke. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudi sasa kwenye suala tunalosema kwamba Walimu wetu hawapati stahiki wanazostahili. Tumeona Serikali imejitahidi, lakini kuna wale walimu ambao kwa kweli wanafanya masomo ambayo yanasababisha wao wakae vipindi zaidi pale shuleni. Naomba hawa walipwe hardship allowance. Mwalimu siku zote alikuwa mtu wa maana sana, mwalimu alikuwa akipita anaheshimika, anasalimiwa kwa heshima, nyumba yenye heshima ni nyumba ya mwalimu, lakini sasa hivi walimu wengi wamedhalilika ile heshima imekwenda wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeona labda irudishe walimu wengine wa sekondari kwenda primary wenzangu wamezungumza, tunaomba wale walimu wa sekondari wanaokwenda primary waandaliwe pia, kwa sababu mwanafunzi akishapata msingi mzuri kama tunavyosema tu nyumba nzuri ni msingi, mwanafunzi akianza hapa chini basi akienda huko juu ameshajiimarisha na ameshajitambua. Naomba sana tuwaanzishie wanafunzi hawa msingi mzuri ili huko wanakoenda sasa waweze kwenda kufanyakazi wakiwa wanajua wanafanya nini. Siku zote elimu haina mwisho, hata wale ambao wameshamaliza Masters wanakwenda kwenye ajira lakini pia wananyanyasika labda kwa vile hawana uzoefu. Naomba ule muda wa kwenda kufanya field iweze kuandikwa kwenye vyeti vyao kwamba amefanya field mahali fulani na amekuwa na ufaulu wa kiasi fulani. Kwa sababu mwanafunzi anapokuja kua-apply kazi kwa mara ya kwanza, swali linakuja ana uzoefu ama experience gani?(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga hoja mkono.