Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, na mimi niweze kuchangia kwenye Bunge lako hili tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa napenda kuwapongeza Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana pamoja na Naibu wake, Mheshimiwa William Tate Olenasha, kimsingi mnafanya kazi nzuri. Niwape moyo, hakuna kazi ambayo mtaifanya mithili ya malaika, sisi ni binadamu kazi yetu ni kukosoa, lakini msife moyo kazi mnaifanya na sisi tunaiona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, alichangia ndugu yangu Mheshimiwa Catherine Ruge, nadhani hayupo, nilipenda angekuwepo naye anisikilize. Alikuita Madam Professor sioni statistics usiogope! Mheshimiwa Waziri unakumbuka niliposimama hapa nililia na wewe nikakuomba hostels za wanafunzi umetupa. Tulikulilia kuhusu Mloganzila umetupa, Mheshimiwa Oscar amekiri pale alikuomba nyumba za Walimu wake umempa. Mheshimiwa Waziri tunataka vitu tangible chini ya Wizara yako, vitu ambavyo tutaviona, hatutadai statistics, tutakudai Ilani ya Chama cha Mapinduzi ilielekeza nini na wewe unafanya nini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri ninakupa hongera, isitoshe ninakushukuru sana kwa kuwa tayari katika kui-support Uni Life Campus Program na kwa hakika tumeona utayari wako katika kutengeneza Taifa linalojiheshimu na taifa ambalo lina uwezo wa kushindana kwenye soko la ajira. Mheshimiwa Waziri pokea pongezi zangu za dhati kutoka kwa wanafunzi wote Vyuo Vikuu nchi nzima. Uni Life Campus Program inazunguka nchi nzima na hii ni feedback ya wanafunzi wao, ni feedback ya walimu, ninakupa pongezi, endeleeni. (Makofi)

Mheshimwa Mwenyekiti, ninasimama kuchangia kuhusu Mfuko wa Bodi ya Mikopo. Nina machache sana ya kuongea katika hili na nitaongea hapo tu sitataka kwenda mahali pengine. Mheshimiwa Waziri, pamoja na pongezi ambazo hata ndugu yangu Mheshimiwa Oscar amezitoa, ni kweli, tumeona mafanikio mazuri sana. Tunapoongelea Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Mheshimiwa Dkt. John Joseph Pombe Magufuli, tumeona kumekuwa na ongezeko kubwa la wafaidikaji wa Bodi ya Mkopo. Utakumbuka miaka kumi, ninapoongelea hivi ninamaanisha mwaka 2005 mpaka mwaka 2015, tumekuwa na wafaidika 390,922 lakini kwa miaka miwili tu 2015 mpaka 2017, tumekuwa na wafaidika wapya 113,922.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri hii ni pongezi ambayo haipaswi kubezwa, sisi tuliokuwa na Ilani ya Chama cha Mapinduzi, tuliokuwa na party manifesto mikononi mwetu tunasema hii ndiyo kazi ambayo tulipewa dhamana na wananchi wetu na sisi tukaitekeleza bila hofu. Makelele haya yasiwatishe, tuna mengi ya kujibu tunapofika mwaka 2020. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hivyo tu, tumeona masuala mazima ya urejeshwaji wa mikopo Bodi ya Mikopo, tumeona kuna hatua kubwa imepigwa. Tunapoongelea katika miaka kumi iliyopita, urejeshwaji wa Bodi ya Mikopo tofauti na alivyokuja Badru, tuliweza kukusanya shilingi bilioni 101 katika miaka kumi, lakini katika miaka miwili tu 2015 hadi 2017, chini ya uongozi wa Ndugu Badru, tumeweza kukusanya shilingi bilioni 285. Kwa kweli Mheshimiwa Waziri hizi ni pongezi zetu kwa Wabunge wa Chama cha Mapinduzi kwa sababu sisi ndiyo wenye Ilani na tunajua kwenye ilani kuna nini.

Endelea na kazi hii kwa sababu huu ni utume wa kanisa na sisi tuna imani na wewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na haya, tunasema kabisa ukiangalia kwenye ripoti ya CAG na ripoti ya Bodi ya Mikopo tunapoongelea katika mwaka 2005 toka uanzishwaji wa Bodi ya Mikopo mpaka muda huu tuliosimama hapa pesa ambayo ilipaswa kuiva na kurejeshwa ilikuwa shilingi bilioni 585 lakini katika pesa hizi, shilingi bilioni 235 bado hazijaweza kurejeshwa. Pamoja na ukusanyaji mzuri lakini zipo pesa ambazo imeshindikana kurejeshwa lakini explanation tofauti na explanation ya CAG Bodi ya ya Mikopo inasema hawa ni pamoja na wanafunzi ambao wako kwenye grace period ya miezi 24.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mnakumbuka hata Wabunge tulipitisha Miscellaneous Amendment ya kutaka asilimia 15 kutoka kwenye asilimia nane, hapa kuna kitu ambacho inabidi tukiangalie, something is alarming. Kwa sababu mwisho wa siku lazima tuone mfuko huu unaweza kujiendesha na ukisoma ripoti ya CAG ziko pesa nyingi hazijaweza kurejeshwa. Sasa tunatoa wapi, vyanzo ni vipi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri nasema something is alarming kwa sababu sioni nguvu ya Serikali ilipojikita katika kuona kwamba vijana hawa wanaajirika kwa wakati. Mheshimiwa Waziri mwaka jana 2017 ukiangalia ikama ya Serikali tulisema tutaajiri vijana 52,000 lakini sad enough tumeweza kuajiri vijana 16,800 sawa na asilimia 32, Mheshimiwa Waziri tunakwenda wapi? Je, tulitengeza ile Paralegals Act katika kuja kutoa hukumu isiyo kuwa na hatia kwa vijana wetu. Mwisho wa siku hawa watapaswa kurejesha pesa hizi, watazitoa wapi endapo Serikali yetu inashindwa kujipanga katika kuandaa ajira kwa vijana wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri ninapoongea suala hili hapa katika Wizara hii ya Elimu utakubaliana na mimi tuna graduates zaidi ya laki sita kwa mwaka, lakini it is less than ten percent wanaingia kwenye ajira rasmi za Serikali. Mheshimiwa Waziri inabidi tukaze buti kuona kwamba vijana wetu tunawaandalia mazingira makini ya wao kuweza kuajirika na kuweza kuona kwamba bodi hii inajiendesha kwa fedha hii kuzunguka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri ukiangalia page ya 15 ripoti ya Waziri Mkuu alisema kwamba ametoa shilingi milioni 783 kwa vijana 840 sawa na asilimia 0.105. Mheshimiwa Waziri sioni mwelekeo kidogo ninapata giza hapa ukiangalia vijana wanaomaliza, wanao graduate na vijana wanaoingia kwenye soko la ajira hata kwa kujiajiri bado hai-reflect nguvu yetu, hai-reflect majibu ambayo tunapaswa kutoa kama wabeba ajenda na kama wabeba Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapoongea suala la VETA ambalo hata dada yangu Mheshimiwa Janet Mbene ameliongelea, VETA is almost dying, Mheshimiwa Waziri ni vema ukaangalia. Ripoti ya CAG page 138 inaonesha kabisa kuna matatizo pale, VETA haijulikani ni regulator, haijulikani ni key player! Anatuambia kabisa ukisoma page ya 138 kwenye chuo kimoja ambacho kilikuwa sampled hapa Dodoma unaambiwa uwiano wa wanafunzi ni moja kwa kwa113, mwalimu mmoja wanafunzi 113! Mheshimiwa Waziri ubora wa elimu unatoka wapi hapa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajiandaa kuingia kwenye Tanzania ya viwanda tunaongea nini katika takwimu hizi. Licha ya hivyo utaangalia kwenye moja ya mipango ya Ofisi ya Waziri Mkuu tumesema tuna programu ya uanagenzi kwa nini programu hii ya uanagenzi katika mwaka huu wa fedha 2018 tumesema wafaidika watakwenda kuwa 10,500. Kwa nini programu hii nguvu kazi ya Taifa inayoelekezwa katika programu hizi tena kwa kupeleka vijana wetu kwenye vyuo holela vya mtaani, mathalani Don Bosco siwezi kuita holela sijui! Hatujui mitaala yake mnapeleka vijana kule kwenda kujifunza kuandaa na Tanzania ya viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba Waziri atakapokuja kuhitimisha mada yake atuambie amejiandaaje kutumia fursa hizi katika kuona kwamba Bodi ya Mikopo inajiendesha, vijana wanaingia kazini akija hapa atuambie nini mipango yake kama Wizara, nini mipango yake kama Waziri mwenye dhamana katika kuona kwamba bodi hii inaweza kujikimu kutokana na fedha ambazo zinatoka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, iko mipango mingi ukiangalia Ofisi ya Waziri Mkuu pia kuna hela nyingi zimewekwa bilioni 15 katika kusaidia vijana waingine kwenye kilimo, umejiandaaje Mama Ndalichako, umejiandaaje Bodi ya Mikopo ili vijana hawa waweze kurudisha pesa? Hizi ni fursa umejipangaje. Ukienda kwenye private sector ambazo tunategemea vijana wengi wanaweza kuajiriwa tazama TBL ni almost imefungwa, wamebaki gate keepers wamebaki, wamebaki watu wachache sana pale, vijana wetu wamekosa ajira TBL, angalia payroll ya TBL inafanyikia Mauritius, kule wana enjoy tax…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)