Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Natambua kwamba leo ni Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari duniani. Napenda kutumia fursa hii kuweza kuwakumbuka wale wote ambao waliweza kupoteza maisha kwa sababu ya kazi yao ya uandishi kama ndugu Mwangosi ambaye aliuawa na Jeshi la Polisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ndugu yetu Azori ambaye mpaka sasa hivi amepotea hatujui yuko wapi; na wengine wote Ansbert Ngurumo sasa hivi yuko uhamishoni kwa sababu ya shughuli ya Uandishi wa Habari na wengine wote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tuko kwenye Wizara ya Mambo ya Ndani na nafikiri tumekuwa tukishuhudia baadhi ya Maafisa ndani ya Jeshi la Polisi, tena wakubwa kabisa wakisema maneno kinyume kabisa cha weledi unavyowataka ndani ya Jeshi la Polisi na hekima kabisa hawana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, inafedhehesha sana kwamba Jeshi la Polisi ambalo kazi ni kulinda raia na mali zao, wamegeuka kuwaona raia kama mbwa koko ndani ya nchi yangu ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa kifungu cha
(32) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai kinawataka Jeshi la Polisi kumfikisha mtuhumiwa Mahakamani ndani ya saa 24. Tumeendelea kushuhudia Jeshi la Polisi ama kwa makusudi au kwa kile wanachokiita maagizo kutoka juu; na sijui ni juu wapi siku hizi kwenye Awamu hii ya Tano, kitu kikifanyika, tunasubiri maelekezo kutoka juu. Sijui ni sheria ipi ambayo wameitunga ambayo haijaletwa Bungeni hapa kuthibishwa kwamba kuna maelekezo yanatakiwa yatoke juu ili Jeshi la Polisi litende kazi kwa mujibu wa weledi wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilipokuwa Gerezani nilikutana na binti anaitwa Salma Ramadhani ambaye alifutiwa mashtaka yake baada ya kukaa miaka minne Gerezani na Mheshimiwa Hakimu Mwijage akatoa ruling kwamba huyo dada asikamatwe na wenzake watatu; lakini alivyotoka tu, akakamatwa baada ya siku mbili akarudishwa Kisutu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yule Hakimu Mwijage akasema, “nimesema huyu mtu asikamatwe mpaka apate kibali cha Mahakama Kuu.” Polisi walimkamata akaenda na wenzake wakaa Kituo cha Kawe zaidi ya miezi nane ndani ya Kituo cha Kawe. Ukaguzi ukiwa unapita, wanawachukua wanakuja wanawaweka pale Kisutu, hawawaingizi ndani ya zile chamber, baadaye wanawarudisha. Hawa Watanzania ndani ya miezi nane.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua hawa Maaskari ambao kuwaweka Watanzania zaidi ya miezi nane kituoni mpaka sasa hivi bado wako nao, watueleze hizi ni sheria za wapi? Ni mambo mengi sana yanatendeka kinyume. Nina muda mchache sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Magereza kuna wastaafu ambao wamestaafu mwaka 2017, mpaka leo hawajawalipa stahiki zao hata fedha za kubeba mizigo hawajawapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine kuna magari 950 mwaka 2012 ambayo yaliidhinishwa kwamba yanunuliwe na yasambazwe nchi nzima kwa ajili ya kubebea mahabusu kwenda Mahakamani. Mpaka leo hayo magari hayajulikani yameota mbawa za wapi. Sasa kwa sababu Awamu ya Tano mna-fight ufisadi, tunataka mliambie Bunge hili, hayo magari yameota mbawa za wapi? Kama yamenunuliwa, yako wapi? Maana yake tunashuhudia ndugu zetu ambao wako Magereza wanabebwa kwenye makarandinga kupelekwa Mahakamani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine ambacho napenda kuzungumzia kwa haraka haraka, tunaomba waweke vifaa vya kisasa kuweza kuwakagua wale watu ambao wanaingia Magereza. Kinachofanyika sasa hivi ni udhalilishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano, mwana mama anakuja anataka aingie gerezani, ana-bleed anaambiwa kama ana-bleed anabidi aruke kichurachura kumchunguza kama ana kitu ameweka ndani au wanamwingiza mkono. Huu ni udhalilishaji, haukubaliki. Nunueni vifaa vya kisasa vya kuweza kuwapima na kujua kama ana kitu, vina- detect. Naomba wanunue vifaa vya kisasa ambavyo ni vya bei rahisi sana, wasidhalilishe Watanzania. Wanunue vifaa vya kisasa waweze kufunga, waweze kukaguliwa wakati wanatoka na wakati wanataka kwenda Mahakamani na wakati wanaingia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Magereza imepitwa na wakati, tunaomba ifanyiwe marekebisho. Leo utashuhudia Askari Magereza ana masters lakini analipwa kama mtu wa Form Four. Pia kuna mengine mengi ambayo yanatendeka kwenye Jeshi la Magereza ambayo ni kinyume. Leo wafungwa hawa uniform. Unakuta wakati mwingine Askari anatoa jezi yake anampa mfungwa. Ni aibu! Wao kama wamepeleka wafungwa, wawahudumie, hawana uniform kabisa. Wanawapa adhabu Maaskari Magereza. Unakuta eti mfungwa ameweka kilemba kimeandika tu “mfungwa” huku hana sare.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kusema kwamba wanatumia nguvu nyingi sana, fedha za Watanzania maskini; wakati wa Ukuta ndiyo tuliona watu wanafanya demonstration na Askari, wakati wa Mange Kimambi tukaona watu wanafanya demonstration ya Askari wajulikane kama wanafanya mazoezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wasiharibu fedha za Watanzania maskini kwa kutembeza Maaskari na magari ya washa washa, hizo fedha wapeleke kwenye mahospitali, hizo fedha wangezi-convert zingeweza kujenga shule. Watoto wanasoma 200 kwenye darasa moja. Leo anaweza akajitokeza mtu amekaa sijui Canada akasema anaanzisha maandamano Tanzania, halafu Serikali inakuwa iko tete.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeshuhudia matamko ya IGP, (Maneno haya siyo sehemu ya Taarifa Rasmi za Bunge) tumeshuhudia matamko ya Mheshimiwa Waziri pale, tukamshuhudia Rais, tukamshuhudia Mkuu wa Majeshi, just a single lady who is sitting in the USA, wanawatetemesha, wanatumia rasilimali zetu vibaya. Wana hofu gani Serikali ya Awamu ya Tano ya Chama cha Mapinduzi?