Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nitaanza mchango wangu kwa kum-quote Nelson Mandela, muda wangu ni mchache sana, amesema; I learned that courage was not the absence of fear, but the triumph over it. The brave man is not he who does not feel afraid, but he who conquers that fear. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kusemaje; tumefika hapa au tunalazimishwa kufika mnakotaka tufike sio kwa sababu hatuogopi, kwa sababu tunalazimishwa kutokuogopa tena. Humu ndani sisi Wabunge wa Upinzani nakumbuka ndio tulikuwa mstari wa mbele kuwatetea polisi, kutetea makazi yao, kutetea matatizo yao, lakini nini kimetokea; polisi wametufikisha hapa, polisi tulikuwa tunawapenda sana na tunawapenda lakini mnakokwenda baba mmepotea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, upolisi ni taaluma na kama walipenda kuwa wanasiasa wangekwenda kugombea kama tulivyofanya sisi. Tunaamini wao ndio wanapaswa kututetea, tunaamini watu ni lazima wajione wako salama mikononi mwa polisi, lakini leo nini kinatokea; ukikamatwa na polisi huna uhakika kama utatoka salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Saguta Heche anakufa akiwa amefungwa pingu mikononi mwa polisi, Akwilina mtoto wa watu akisafiri kwenye daladala, anashutiwa na kufa na polisi na tunakuja kuambiwa hatujaweza kumtambua nani polisi kamuua kwa hiyo faili limefungwa. Mnatupeleka wapi ninyi watu? Tunawapa fedha kutoka kwenye kodi ya nchi hii, polisi tunawapenda lakini mlikotufikisha siko tulikokutamani. Narudia kusema tunaamua kuwa courageous sio kwa sababu sisi sio waoga ila kwa sababu mmetulazimisha kufika hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina case study ya polisi mmoja ambaye alimvamia mtu wangu wa karibu na Mheshimiwa Waziri nilimpigia simu nikakwambia mume wangu amekuwa attacked na polisi anayenifahamu mimi, anaishi kwenye mtaa wangu, yule polisi amemwonea yule baba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimetoa taarifa kwenye kituo kikuu cha polisi, nimekwenda mbali zaidi nimekwenda hata kwa Mnadhimu wa Polisi, bw. Matiko Central, barua ninazo hapa, tangu 2017 hakuna kitu kilichofanyiwa kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachokiona, uozo wa polisi wanaouona chini ni kutoka chini mpaka juu. Kama kiongozi mdogo, afisa wa polisi amekosea, unakwenda kwa bosi wake amrekebishe, unakwenda kwa Waziri, Waziri alinipa pole, lakini pole inasaidia nini kama tunawaacha wale vijana wanazidi ku-harass watu wasiokuwa na hatia mtaani kwa sababu tu alikuwa kwenye bodaboda na walikuwa hawajavaa helmets. Ni kazi ya polisi kukamata na kupiga watu kwa sababu hawajavaa helmets? Come on guys! Come on guys! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niambieni kama Polisi wetu hawaelewi miiko na kazi yao kutokana na maandishi yao na vitabu vyao vya PGO’s naomba muwafundishe. Walipotufikisha ndio maana tunaongea haya yote, siyo kwa sababu hatuwapendi, ni kwa sababu wameondoka wenye msingi. Turudi kwenye masuala mazima ya maadili ya Jeshi la Polisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani tunajua tunapokuja hapa tunachopaswa kuongelea ni weledi wa Jeshi la Polisi, ni namna gani linafanya kazi, ni namna gani inatumia kodi tunazowapatia na ni namna gani ina-deal na raia? Those are the things you must be talking here. Hatupaswi kuwasifia, kufanya kazi ni wajibu wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tunachokitaka ni kuangalia makandokando yao na namna gani tunaweza kuwarekebisha kwenda mbele. Wamegeuka wanasiasa, wamegeuka wapiga debe wa Chama cha Mapinduzi. Nani hataki?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kuwaambia Jeshi la Polisi, sisi tukiingia madarakani, tunawahitaji, tutawatumia wao. Hata hivyo, hatutaki watupe favour sisi dhidi yenu ninyi, tunaka wasimame katika kama referee. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, namalizia kusema, mmomonyoko mkubwa wa maadili ya Jeshi la Poilisi nau- associate na kumhujumu Mheshimiwa Waziri Mwigulu Nchemba. Naamini pengine hawamtaki Mheshimiwa Nchemba. Ni kwa nini tunaona Jeshi la Polisi wanafanya mambo ambayo hatujawahi kuyasikia katika historia ya Taifa hili? Pengine Mheshimiwa Waziri labda ukijiuzulu tunaweza tukapona. Wewe unaonaje? Pengine ukijiuzulu tutaweza kupona. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nam-quote Che Guevara, aliwahi kusema: “If you tremble with indignation at every injustice then your comrade of mine.” Kama dhamira yako Mheshimiwa Waziri inaguswa na matendo ya Jeshi la Polisi na Maafisa wa Jeshi la Polisi, tunataka tukuone ukichua hatua dhidi ya hao maharamia wanaochafua Jeshi la Polisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.