Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, napenda kuchangia kuhusu usikivu wa Redio Tanzania. Nkasi Kusini eneo Tarafa ya Wampembe kandokando ya Ziwa Tanganyika hawapati matangazo ya TBC na hali hii inawasononesha sana. Naomba Serikali ilifanyie kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, nashauri gharama za matangazo mbalimbali ipungue kwani wananchi wangependa kutangaza matukio mbalimbali lakini tatizo ni gharama. Hata biashara hazikui kwa kasi bila matangazo. Kumbe gharama zikipungua uchumi wa wananchi utaweza kukua na kuwezesha nchi na wananchi wake kuishi maisha yaliyo bora.