Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia Wizara hii kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la wavuvi wa Mafia ni kule kuambiwa wahame eneo wanalovulia miaka mingi na kufanywa Hifadhi ya Taifa, hivyo wananchi kukosa eneo la uvuvi. Naishauri Serikali kuangalia upya jinsi ya kuwatafutia wananchi eneo la uvuvi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la majosho kwa ajili ya wafugaji wa Mkoa wa Pwani, Wilaya ya Kibaha, eneo la Kwala ambako wafugaji wengi Wakwavi, Wamasai wanapoteza mifugo yao mingi na ECF (Ndigana Baridi) kutokana na kukosa majosho na dawa za mifugo kuwa juu. Nashauri Serikali irudishe mpango wa ujenzi wa majosho ili kusaidia wananchi. Pia kuwepo punguzo la bei ya dawa ili kusaidia wananchi kumudu gharama.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia nashauri kusaidia udhibiti wa soko la mazao yatokanayo na mifugo, mfano, kuku wa nyama kuletwa kutoka nchi za jirani hivyo kuua soko la ndani la wafugaji. Mfano, wafugaji wa kuku wa mayai wanakosa soko la mayai kutokana na mayai toka nchi za jirani kuingia nchini.