Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, napenda kuongelea kuhusu madeni ya matangazo kwenye magazeti ya Serikali. Sikuona busara kulisema hili hadharani, kiukweli Wizara na Taasisi za Umma zinadaiwa mamilioni ya fedha za matangazo kwenye magazeti ya Daily News na Habari Leo. Je, huko kwenye private media kama Mwananchi, The Guardian, The East African ni kweli kuwa Wizara na Taasisi hazilipii hayo matangazo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika nyakati hizi ambazo social media imekuwa fast kueneza na kusambaza taarifa ipo sababu kuyawezesha magazeti ya Serikali kwa kulipa madeni ya matangazo ili vyombo hivyo viweze kuendelea kuwekeza na kukabiliana na private media ambazo kwa nguvu ya fedha zinaweza kuwa chanzo cha upotoshaji wa taarifa. Nyote mnajua nguvu ya media, hatuwezi kukwepa kuwezesha vyombo vyetu japo kwa kulipa madeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ving’amuzi Vs free channel. Kwa nini wenye ving’amuzi hawaachii free channel tano kama miongozo inavyoelekeza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.